Posts

Showing posts from November, 2023

Jinsi Ya Kupanga Na Kufanikisha Malengo Yako…

Image
Kitu unachopaswa kujua ni kwamba kuazimia malengo ni kitu kingine na kufanikisha lengo ni kitu kingine. Lengo likiazimiwa haimaanishi kwamba ndiyo limetimia. Hivyo basi ili kufanikisha lango lako hatua zifuatazo ni lazima zizingatiwe kwanza:- ➡️Andika Malengo Yako… Ili kutimiza malengo uliyoyaazimia ni lazima uyaandike kwanza. Unachopaswa kujua ni kwamba ili lengo liitwe lengo sharti ni lazima liandikwe… hii ni kwa sababu lengo ambalo halijaandikwa huwa ni tamanio tu ambalo haliwezi kutimizwa.  Unatakiwa uandike kwa sababu akili yako huwa inaingiza taarifa nyingi, kwa mantiki hiyo lengo lisilioandikwa ni rahisi kusahaulika.  Hivyo basi ili kutimiza lengo lako ni lazima uliandike na kulisoma kila siku kabla ya kulala na ukishaamka. Mbali na hilo unahitaji kuandika malengo yako kwa sababu kuandika kunakufanya utengeneze kitu Fulani unachoweza kukishika na kukisoma kila unapohitaji kukisoma.  Kadhalika unapoamua kuandika lengo lako utajikuta ukiunganishwa na kanu...

Huwezi Kubadili Kesho Yako Mpaka Usome Kwanza Hii..

Image
Hivi unajua kwamba kesho yako inatabirika kulingana na hali yako uliyonayo leo pamoja na kile unachokifanya? Unatakiwa kujua kwamba, kama vil e mama mjamzito anavyokadiriwa kuwa atazaa baada ya miezi tisa. Vivyo hivyo ndivyo ilivyo kwa kesho yako.  Hii ni sawa na kusema kuwa, kesho yako inatabirika kulingana na hali yako ya leo! Mbali na hilo kanuni ya makadirio inasema kwamba; “kwa kila tukio linalotokea kuna uwezekano kuwa tukio hilo hutokea kutokana na hali fulani.”  Tukihusisha kanuni hii na kesho yako, tutasema kesho yako inatabarika kupitia hali uliyonayo leo pamoja na kile unachokifanya. Kwa minajiri hiyo kile unachokifanya leo, ndicho kimebeba thamani ya kesho yako! Hata hivyo kabla sijaenda mbali zaidi unatakiwa ujiulize swali hili, "vipi kama hali niliyonayo leo itaendelea kuwa hivihivi pamoja na hiki ninachikofanya leo kikaendelea kunipa matokeo haya haya?" Je, maisha yangu baada ya miaka kumi yatakuwaje?  Sijajua upo katika hali gani. Lakini jibu u...

Jinsi Ya Kujitengenezea Na Kujiongezea Thamani Sokoni...

Hivi unafahamu kwamba thamani ya mtu ndiyo hupima hadhi yake pamoja na kipato anachoweza kukitengeneza?  Unatakiwa kujua kwamba utabadili maisha yako siku utakayoamua kuongeza thamani Yako! Na kama hutoamua Kujiongezea  thamani hakuna atakayekufanyia hivyo!  Hata hivyo unatakiwa kujua kwamba, siku ambayo thamani yako itapanda, ndiyo siku ambayo ulimwengu utakutambua wewe ni nani! Hakuna kipya chini ya jua, maandiko matakatifu yanasema hivyo!  Hii inamaanisha kwamba kwa chochote kile utakachokifanya, tayari kuna watu walishafanya, lakini pia kuna wengine ambao wanafanya kitu hichohicho na kwa namna moja ambayo hata wewe unafanya!  Hivyo basi ili kufikia hatua ya kutambuliwa na watu wengine, ni lazima uwe umejiongezea thamani kubwa sana, kiasi kwamba utaweza kutofautishwa na wengine!  Kwa ujumla thamani ni kipimo rasmi ambacho, humstahilisha, humheshimisha pamoja kumtambulisha mtu! Je, kwa namna unavyojiona, wewe ni mtu wa thamani? Je, umeweza kutengeneza tha...