Posts

Showing posts from October, 2023

Usimtendee Mwenzako Yale Usiyependa Utendewe Na Wewe "The Golden Rule"...

Image
Hivi unafahamu kwamba Moja ya sababu kubwa ya magumu ambayo wanadamu tunakutana nayo ni kwa sababu ya kukosekana kwa upendo baina yetu? Ukweli ni kwamba, tungekuwa tunawatendea wenzetu yale ambayo tungependa sisi wenyewe tutendewe, basi kusingekuwa na chuki, hasira, vinyongo pamoja na visirani. Lakini haya yote yametapakaa katika kizazi hiki cha leo, kwa sababu tunawatendea wenzetu yale ambayo sisi wenyewe hatupo tayari tutendewe, na endapo itatokea tumetendewa basi tunaanza kuchukia na kujenga hasira kali vifuani mwetu! Mhubiri 7:9 Neno la Mungu linasema; “Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, kwa maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu” Rafiki unatakiwa kujua kwamba, hasira huwa haimletei madhara yule anayechukiwa bali humuumiza zaidi yule anayechukia.  Hii ni sawa na kusema, ukiwa na hasira maana yake una fikra hasi kichwani mwako, na hiyo fikra hasi ndiyo inakufanya uwachukie wenzako pamoja na kuwatendea yale ambayo wewe mwenyewe hupendi kutendewa!   Hebu j...

Fahamu Kuhusu Sehemu Mbili Za Akili Na Jinsi Utendaji Kazi Wake Unavyopima Kila Kinachotokea Maishani Mwako…

Image
Hivi unafahamu kuwa unamiliki akili moja ambayo hufanya kazi kwa kutumia sehemu kuu mbili tofauti za akili, huku  utendaji kazi huo ukiwa ndiyo hupima kila kinachotokea maishani mwako? Ukweli ni kwamba, watu wote wanamiliki akili, lakini ni watu wachache sana kati ya hao ndiyo wanajua jinsi gani akili zao zinafanya kazi!  Laiti kama kila mtu angejua jinsi gani akili yake inavyofanya kazi, huenda tusingekuwa na dunia hii tuliyonayo sasa na huenda tungeishi maisha ya hadhi nyingine kabisa! Makala hii fupi itaenda kudokeza jinsi akili yako hufanya kazi, na jinsi gani utendaji kazi huo huathiri kila kibnachotokea maishani mwako, ikumbukwe karibu kila kitu kinachotokea maishani mwako huanzia akilini mwako! Mpenzi msomaji unatakiwa kujua kwamba unamiliki akili moja ambayo hufanya kazi kwa kuhusisha sehemu mbili tofauti za akili, na ufanyakazi wa sehemu hizo mbili huongozwa na kanuni ya kuamini. Sehemu ya kwanza inaitwa Conscious Mind; hii ni sehemu ya akili ambayo huchuk...

Fahamu Sababu Kuu Moja Kwanini Sala Na Maombi Huwa Hayajibiwi Kama Ulivyotarajia...

Image
Hivi unafahamu kuwa dhambi ndicho chanzo kikuu cha maombi mengi kutokujibiwa kama yalivyotarajiwa na muombaji? Ukweli ni kwamba hakuna kitu kingine ambacho huua mawasiliano baina ya mtu na Mungu zaidi ya kuliko, unatakiwa kujua kwamba dhambi huua kabisa ule muunganiko uliopo kati ya Mungu na mwanadamu, na endapo uhusiano baina ya pande hizo mbili utakuwa haupo inamaanisha kwamba pande hizi mbili haziwezi kusikilizana. Kutokana na ukweli huo huna budi kuweka akilini mwako kuwa, hata kama utaomba kwa namna gani kama mawasiliano kati yenu yametenganishwa na dhambi Mungu hawezi kukusikiliza kabisa!. Nini ufanye? Unachopaswa kufanya ni kuacha dhambi na kuanza kuuishi usafi wa roho. Na ndiyo maana katika kitabu cha Ayubu 22:23 Neno la Bwana linasema; “Ukimrudia Mwenyezi, utajengwa upya; ukiuondoa udhalimu ndani ya hema yako”. Rafiki unatakiwa kujua kuwa, haumrudii Mungu kwa kutamka tu kwa mdomo wako, bali unamrudia mungu kwa kuondoa udhalimu (kuacha dhambi), ukishaacha dhambi tu ...

Furaha Huweza Kuponya Yote, Furahi Kwa Sababu Yote Ni Mapenzi ya Mungu...

Image
Hivi unafahamu kuwa huzuni imeweza kuwamaliza watu wengi kwa kuwakosesha raha pamoja kuuondoa kabisa ule umuhimu wa maisha yao hapa duniani? Huenda hata wewe ukawa ni yule mtu ambaye kwa muda mrefu umekuwa ukihuzunika na ushapoteza kabisa tumaini la kuishi tena! Ukweli ni kwamba furaha ndilo lengo kuu la kila binadamu, na hii ni kwa sababu kila mtu hufanya jambo fulani ili kutimiza furaha yake.  Kwa mantiki hiyo huzuni siyo jambo la kulivumilia kwa kuwa hakuna mtu mmoja ambaye hufanya jambo fulani ili apate huzuni, bali wote hufanya mambo mengi ili kutimiza furaha zao! Hii ni sawa na kusema ili uweze kuwa na maisha yenye amani ni lazima uikatae huzuni kwa nguvu zote na uitafute furaha kwa juhudi zako zote! Na ndiyo maana,  Zaburi 37:4-5 Neno la Mungu linasema;  “Nawe utajifurahisha kwa Bwana, naye atakupa haja za moyo wako, Umkabidhi Bwana njia yako, pia umtumaini naye atafanya” Mpenzi msomaji unatakiwa kujua kwamba kuna baadhi ya mambo ili Mungu apate kukuten...

Hivi Ushawahi Kujiuliza Kwanini Huwa Unapata Kinyume Na Kile Ukiombacho?...

Image
Mbali na kuwa watu wengi tumefundishwa kuamini juu ya kile tukiombacho, lakini wengi wetu tumeishia kupata kinyume cha kile tukiombacho.  Laiti kama kila sala ingekuwa huwa inajibiwa kama vile muombaji anavyotaka basi hapa duniani kusingekuwa na shida, taabu, mateso, mahangaiko, maradhi, magonjwa n.k.  Na kila mtu angekuwa anafurahia maisha yake. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba asilimia kubwa ya watu hupata kinyume na kile wakiombacho, huku sababu kubwa ikiwa ni kutokujua kanuni ya sala inayojibiwa ni ipi! Makala hii fupi inaenda kudadavua suala hili kiundani, na nina uhakika endapo utasoma mpaka mwisho, utaweza kujifunza jambo kubwa sana ambalo hukuwahi kujifunza hapo awali... Mathayo 18:19;  “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lolote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni”. Uelewa hafifu wa kifungu hicho, umeleta utata sana linapokuja suala la kuomba.  Kwamba mtu anajikuta akiomba jambo Fulani la...

Je, Ushawahi Kujiuliza Juu Ya Haya...?

Image
Kwanini mtu mmoja ana furaha ilihali mwingine ana huzuni?  Kwanini mtu mmoja anapona ugonjwa ambao unasadikika hauwezi kuponywa ilihali mwingine haponi?  Kwanini mtu mmoja ana hofu, wasiwasi, hana amani, hana tumaini ilihali mtu mwingine ana furaha, amani na matumaini? Kwanini mtu mmoja anafanikiwa katika jambo Fulani ilihali mtu mwingine anashindwa kufanikiwa katika jambo hilo? Kwanini mtu mmoja anafanikiwa kujibiwa katika sala juu ya jambo Fulani ilihali mwingine anashindwa kujibiwa katika jambo hilo? Kwanini watu wengi wanaosali sana hupitia mitihani, mateso magumu akilini mwao na maishani mwao mwote? Je, kuna majibu yoyote juu ya haya? …muda siyo mrefu utaenda kuujua ukweli.  Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, na hiyo kweli itawaweka huru”. Huenda ukawa unapitia nyakati ngumu sana kiasi kwamba umeshakata tamaa na huna tumaini lolote lile… Na, huenda unapitia hali ngumu kama alivyopitia mwandishi wa Zaburi 6:6, ambapo Neno la Mungu linasema; “Nimechoka kwa...

Fahamu Mbinu Kuu Moja Ambayo Hutatua Kila Tatizo...

Image
Moja ya kosa kubwa ambalo watu wengi hufanya wakikumbana na shida, tatizo, maradhi, majanga au hali ya sintofahamu ni kulaumu! Na, hapa ndipo utamkuta mtu akilaumu kuhusu tatizo lililotokea pamoja na kuwalaumu ndugu, marafiki, serikali na lawama nyingine ambazo huelekezwa kwenye kila kona! Ukweli ni kwamba, lawama huwa haitatui shida/tatizo badala yake hulifanya liende katika hatua mbaya zaidi, kwani mtu ambaye anawalaumu wenzake, hujihesabia haki kwa kujiona yeye siyo chanzo na hajahusika kabisa kwa kilichotokea badala yake sasa huwaona  wengine ndiyo tatizo huku tatizo akiwa ni yeye mwenyewe! Ndugu, unatakiwa kujua kwamba, hakuna kiwango cha lawama ambacho hubadili tatizo lililopo au shida iliyopo, bali unaweza kubadili mtizamo wako ulionao juu ya jambo hilo! Sasa basi, badala ya kulaumu, unatakiwa ujipe tathimini ya kutosha juu kile ulichofanya mpaka hilo jambo hilo likatokea huku ukihusisha na kile ambacho Mungu kasema kuhusu jambo hilo kwenye neno lake! Ukweli ni k...

Kama Utaweza Kubadilisha Mfumo Wako Wa Kuamini Nitakuonesha Jinsi Ya Kumaliza Matatizo Sugu Kwa Kutumia Neno La Mungu...

Image
Watu wengi wanajua wanachokitaka maishani mwao, lakini hawajui jinsi ya kukipata pamoja na kukivuta kitu hicho kije maishani mwao! Ukweli ni kwamba watu wengi wamechoshwa na hali wanazopitia, lakini imani yao kuhusu hali hizo haijabadilika hali ambayo imepelekea matatizo hayo yaendelee kuwa sehemu ya maisha yao! Makala hii fupi itaendelea kudadavua hili kwa undani, na nina uhakika endapo utasoma mpaka mwisho kuna kitu kitabadilika maishani mwako, nimekuombea kwa Mungu ili mapenzi yake yatimizwe katika maisha yako! Rafiki kwa kila hali utakayokutana nayo hutakiwi kuangalia ukubwa wa tatizo lako (huo siyo wajibu wako), bali wajibu wako unatakiwa uwe kuangalia ukuu wa Mungu wako dhidi ya tatizo hilo.  Kwa sababu kwake yeye kila jambo linawezekana. Naye ni Mungu wa yawezekanayo na siyo Mungu wa yasiyowezekana! Kutokana na hilo ndiyo maana mwandishi wa kitabu cha Ayubu 22:21 anasema;  “Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndivyo mema yatakavyokujia” Kumbe kumjua Mungu ni c...

Fahamu Kuhusu Fikra Ambazo Humuendesha Mwanadamu Aidha Afuje Fedha Zake Au Awekeze Pindi Akitengeneza Pato...

Image
Jambo la kwanza unalopaswa kujua ni kwamba hakuna binadamu ambaye huzaliwa akiwa na Fikra fulani, bali kila mtu amekuwa na mtizamo wa kuona mambo kwa namna fulani kutokana na yeye alivyo pamoja na namna alivyozoeshwa! Mbali na hilo unatakiwa kujua kwamba hivyo ulivyo, hapo ulipo pamoja na hali uliyonayo kiuchumi ni kutokana na wewe mwenyewe! Hivyo basi kabla sijaenda mbali zaidi somo la leo ngoja tufafanue vipengele vifuatavyo, ni matumaini yangu kwamba vitapanua uelewa wako...  Fikra: ni ile namna ya kufikiri,  hali ya kutizama na kuyaona mambo kwa namna fulani fulani hivi pamoja na kuyapa tafsiri kutegemeana na vile ulivyoyaona... Uwekezaji: ni mfumo utakaokusaidia uweze kuzalisha pesa zako na kuzifanya ziwe nyingi zaidi!  Aseti (Mali): ni kile kitu ambacho thamani yake inazidi kuongezeka kadri muda unavyozidi kusonga mbele...  Au  Aseti: ni kitu ambacho kinaingiza pesa mfukoni mwako! Hii inamaanisha aseti inafanya pesa iendelee kuongezeka mfukoni ...

Onyo! Hata Usifikirie Kuhusu Kubadli Hali Yako Ya Kifedha Mpaka Usome Kwanza Hii...

Image
Hivi unafahamu kwamba mafanikio katika eneo lolote lile maishani mwa binadamu huanzia kichwani mwake? Katika hali ya kawaida huwezi ukapata kitu ambacho kichwani mwako hujakiwazia au hata kufikiria kwamba utakipata! Hii  ni sawa na kusema, watu wengi hatufanikiwi KIFEDHA kwa sababu hatuna fikra za uwezekezaji! Ukichimba kwa undani utagundua kwamba, kitu kilichopo vichwani mwetu ni ile dhana ya kudhani, fedha ilitengenezwa ili ije itumike tu! Huku ukweli kuhusu fedha ukiwa ni ule unaodai kuwa, fedha ilitengenezwa ili ije  iwekezwe au izalishwe!  Kwa mantiki hiyo endapo itatokea huizungushi fedha yako au hujaiwekeza huwezi kutengeneza fedha nyingine hali ambayo itakufanya ushindwe kufanikiwa kufedha! Siyo kwamba watu wote wanapenda kutokuwekeza fedha zao ili zijilizalishe, bali wengi wetu tumejikuta tukifanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali, huku sababu yenye mashiko zaidi ikiwa ni athari ya malezi tuliyokutana nayo. Tafiti za kisaikolojia kuwahi kufanyika z...

Tahadhari Huwezi Kumuabudu Mungu Katika Roho Na Kweli Mpaka Usome Kwanza Hii…

Image
Hivi unafahamu kwamba siyo kila sehemu ambayo jina la Mungu linatajwa inamtangaza Mungu halisi? Unatakiwa kujua kwamba, siku hizi kuna ongezeko la manabii wa uongo ambao wanatumia jina la Mungu ndivyo sivyo na kuwaongoza watu nje na ufalme wa Mungu. 2 Wakorintho 10:13-15 Neno la Mungu linasema; “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu. Maana hata shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawa na kazi zao” Mpenzi msomaji kutokana na andiko hilo unatakiwa ujifunze kwamba, katika sehemu za ibada kuna watumishi wa shetani ambao wamejigeuza tu lakini kiuhalisia hawamtangazi Mungu wa kweli. Na, na ndiyo maana katika injili ya Mathayo 7:15 Yesu anasema; “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali” Kama utakuwa...