USIISHI KWA SABABU ZA WENGINE KAMA HUJAZIELEWA SABABU ZAKO
Anayekusukuma ufanye jambo fulani mara nyingi huwa hakuambii kwa upendo, bali kwa kutaka kukuona ukifanana na wengine. Anajisitiri nyuma ya neno ushauri, ili siku ukiharibikiwa, akae pembeni akucheke kimya kimya. Utasikia wakisema: “Umri umeenda, oa/olewa—unasubiri nini?” “Wenzako wa umri wako wamejenga, wana familia, wana maisha—na wewe je?” Wanaposema hivyo, hawajui jambo moja muhimu sana: kila MTU ana sababu zake za kuishi, na sababu hizo hazifanani. Tofauti hizo si kasoro— ndizo zinazokamilisha uhai wa sisi Watu. Sababu za UWEPO wangu si sawa na zako. Ninachokifanya mimi hapa si kila MTU anaweza kufanya. Na hilo lina maana moja tu: zipo sababu maalumu zinazonizunguka zinazonilazimisha nifanye ninachofanya. Nimesoma na wenzangu shule ya msingi, hawafanyi ninachokifanya. Sekondari—hawafanyi. Advance—hawafanyi. Chuo—hawafanyi. Wafanyakazi wenzangu—hawafanyi. Hata tunaokaa nao—hawafanyi. Kiufupi, wananishangaa. Wamebaki midomo wazi. Wananiona si MTU wa kawaida. K...