jinsi Ambavyo Kazi Za Fasihi Na Baadhi Ya Mafundisho Ya Dini Hupelekea Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...
Pasi na shaka una uelewa Fulani hivi kuhusu kazi za fasihi. Hata hivyo miongoni mwa tafsiri nzuri sana ninayoipenda ya fasihi ni ile inayosema; “fasihi ni kazi ya Sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii iliyokusudiwa” Ukweli ni kwamba kwa kipindi cha muda mrefu, fasihi imekuwa ikitumika kama nyenzo ya kufikisha ujumbe kwa jamii hususani kuhusu masuala Fulani Fulani hivi yanayoendelea kwenye jamii inayohusika! Habari mbaya na za kuhuzunisha zaidi ni kwamba, fasihi ya leo imeacha desturi yake ya muda wote! Yaani kutoka kwenye kuikomboa jamii kifkira kwa kuionya, kuielimisha na kuiasa hadi kufikia hatua ya kuanza kuipotosha jamii! Na hii ndiyo sababu kubwa jamii imeweza kupotezwa na kuanza kushangilia uozo na uovu! Na ndiyo maana siku hizi nyimbo zisizo na maudhui yanayojenga zimekuwa zikikubalika zaidi ukilinganisha na zile nyimbo zenye maudhui yanayojenga na kumkomboa mtu Kifikra! Hebu jaribu kuvuta picha mambo yanayooneshwa kwenye video mbalimbali z...