Je, Siku Kuu Ya Krismasi Inatambuliwa Kwa Mujibu Wa Maandiko Matakatifu?...
Bila shaka ulishawahi kujiuliza kwanini tarehe 25 disemba ilitengwa iwe ndiyo sikukuu ya krismasi, yaani iwe siku maalumu kwa ajili ya kusheherekea kumbukizi la kuzaliwa kwake Yesu, na huenda mbali na kujiuliza hivyo hukupata jibu. Na kama hujawahi kujiuliza basi leo tuuangalie uhalali wa maadhimisho ya siku kuu hii! Angalizo: Sipingani na Imani ya mtu na wala sitaki mtu aachane na imani yake, hata hivyo sikulazimishi uamini kile ninachokiamini mimi. Lengo langu ni kuleta mjadala utakaoibua mtizamo mpya kuhusu mahusiano ya tarehe 25 disemba na kuzaliwa kwake Yesu! Ukweli ni kwamba hakuna andiko lolote lililotuamuru tufanye kumbukizi ya kuzaliwa kwa Yesu tarehe 25 Disemba kila mwaka! Na kama hakuna andiko maana yake siku hii iliamriwa tu na mwanadamu mwenyewe. Na ikiwa mwanadamu ndiye aliyeitenga tarehe hii, maana yake Mungu hayatambui maadhimisho haya. Ninasema Mungu hayatambui maadhimisho haya kwa sababu hakuna sehemu kwenye maandiko yake ambayo katuamuru ...