Posts

Showing posts from July, 2024

Jinsi Ambavyo Mtizamo Wa Kijamii Hupelekea Wanaume Waendekeze Ngono....

Image
Vile jamii inavyomuona na kumchukulia mwanaume ndivyo inavyomfanya awe hivyo. Unatakiwa kujua kwamba huwa hauoni kitu kama kilivyo, bali huwa unakiona kitu kutokana na wewe ulivyo na jinsi ulivyoaminishwa kuhusu kitu hicho.  Na ifahamikie kuwa, utaonesha mwitikio fulani kuhusu kitu hicho kutokana na fikra ulizonazo pamoja na Imani uliyonayo kuhusu kitu hicho. Na hii ndiyo sababu kubwa inawafanya wanawake wengi wa leo wasiwaamini kabisa wanaume kuwa wanaweza kutulia na mwanamke mmoja.  Kwa sababu hiki ni kitu kilichomo ndani ya fahamu zao, na siyo rahisi kuweza kukitoa kwa sababu hicho ndicho wanachokijua na ndicho wanachokiamini! Kwa mfano jamii inamuona mwanaume kama mtu anayetakiwa; atunukiwe ngono kila anapohitaji haijalishi anahitaji kwa nani, mtu ambaye hawezi akakaa miezi mitatu bila kukutana na mwanamke, (na endapo itatokea hivyo anaweza kuwa chizi). Mtu ambaye huwa hatosheki kimapenzi, mtu ambaye ni kawaida kuwa na wanawake wengi, na mengine mengi kama hayo...

Je, Ulishwahi Kujiuliza Kwanini Wanaume Wengi Huhalalisha Ngono? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii...

Image
Si mbaya endapo nitaanza na usemi usemao; “kila kitu hutokea kutokana na sababu”.  Hii ni sawa na kusema kuwa, "hakuna mwanaume hata mmoja ambaye huhalalisha kuwa ngono ni kila kitu kwake na hawezi kutosheka na mwanamke mmoja bila sababu iliyopelekea awe na mtizamo huo." Na ukifuatilia takwimu za duniani kote utabaini kuwa, sehemu kubwa ya dunia ni kama imehalalisha kuwa mwanaume anastahili alale na kila mwanamke atakayekatiza mbele yake, amsaliti hata mke/mwenzi wake na afanye ngono kila anapotaka na kwa kila mwanamke atakayemtaka! Jambo hili limehalalishwa tu na watu wamelipokea na kuliamini chini ya mwamvuli wa "wengi Wape" lakini ukifanya uchanganuzi yakinifu utagundua kwamba siyo kweli! Bila kukupotezea muda ngoja nikakusogeze kwenye sababu ambazo huwafanya wanaume wengi wawe na mtizamo huo:- 1. Nadharia Ya Kibaiolojia Huungwa mkono na tafiti za kisayansi. Nadharia hii hudai kuwa mwanaume huchochewa kufanya ngono kwa sababu ya maumbile yake ya uzazi...

Ukuu Uliobebwa Na Mwanaume Ni Mkubwa Sana Haupaswi Utumike Kubadilishana Na Ngono....

Image
Hivi unafahamu kuwa Mwanaume ni mtu mkuu sana ambaye jamii nyingi hujivunia uwepo wake?  Endapo utazunguka katika jamii nyingi ulimwenguni kote utagundua kuwa, mwanaume amefanywa kuwa kama kichwa.  Hii inamaanisha kuwa mwanaume ni mtawala, mwenye mamlaka na mbeba maono wa dunia ya sasa na hata ile ijayo!  Vilevile tafiti nyingi kuwahi kufanyika zimeonesha kuwa hata ugunduzi mkubwa wa kisayansi wa maeneo kadha wa kadha umefanywa na mwanaume! Hata hivyo ukija kwenye maandiko matakatifu utagundua kwamba mwanaume ndiye aliyepewa ukuu.  Hii ni kwa sababu yeye ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuumbwa na kupewa mamlaka kutoka kwa Mungu. Na tunaona Mungu akamuahidi kuwa atamfanyia msaidizi.  Kwa kusema hivyo kumbe mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanaume. 1 Wakorintho 11:8-9 Hivyo basi, kama mwanaume huna budi ujitambue wewe ni nani, uko wapi, unaenda wapi na umebeba kusudi gani maishani mwako. Ikumbukwe wewe ni kichw...

Fahamu Kuhusu Aina MBILI Za Wanaume Pamoja Na Utofauti Wa Mitizamo Yao Hasa Linapokuja Suala La Ngono...

Image
Si haba endapo utakuwa uliona baadhi ya machapisho yaliyoanisha aina kadhaa za wanaume kwa kutumia vigezo fulani fulani hivi, na pengine labda hujawahi kukutana kabisa na hizi aina MBILI zitakazojadiliwa hapa! Hilo si jambo la kushangaza, kwa sababu hata jambo linaloibuliwa hapa huenda halijawahi kuibuliwa, na endapo liliibuliwa huenda namna lilivyojadiliwa siyo sawa na litakavyojadiliwa hapa! Na ifahamike kwamba, hapa ninaainisha aina MBILI za wanaume kwa kuangalia mitizamo iliyopo kati yao hususani katika eneo Zima la ngono!  Kwa maana wengi wanaona kuwa; "ngono kwa mwanaume ni kila kitu na hakuna mwanaume anayetosheka na mwanamke mmoja" Kwa kusema hivyo nitaenda kujadili hili kwa kutumia kigezo cha kiumbo na kigezo cha kiakili na ukomavu wa kihisia, ambapo tunapata aina kuu mbili za wanaume, ambazo ni:- 1.Wanaume-Wavulana: hii ni jamii ya wanaume ambao kiumbo wanaonekana ni wanaume, lakini kiakili na kihisia hawajakomaa. Mawazo ya wanaume hawa ni ya kitoto wala...

Kama Unataka Kujua Uhalisia Wa Mwanaume Dhidi Ya Dai lisemalo; "Hakuna Mwanaume Anayeridhika Na Mwanamke Mmoja" Soma Hii...

Image
Hivi una Habari kuwa karibu robo tatu ya dunia nzima imehalalisha kuwa ngono kwa mwanaume ni kitu cha kawaida sana kukifanya, kiasi kwamba mwanaume kamili hawezi kukaa bila kufanya ngono haijalishi yupo kwenye mahusiano halali au laaah? Dai hili huungwa mkono na nadharia tete ya kisayansi inayodai kuwa; "kwa mwanaume ngono ni lazima kwa sababu ya maumbile yake ya kibaiolojia yalivyo".  Hivyo huona si kawaida mwanaume kukaa bila kufanya ngono kwa muda mrefu, na katika kufanya makadirio yao, wengi huishia kukadiria kwamba mwanaume hawezi kukaa miezi mitatu bila kufanya ngono.  Kinachostaajabisha Zaidi ni kwamba, hakuna uthibitisho juu ya dai hilo, huenda kuna mtu mmoja alikaa tu mahali na wazinzi wenzake. Wakabuni hilo wazo, baadae akaja na wazo hilo akawauzia wanaume, na wanaume nao wakalipokea na wakalihalalisha iwe ni falsafa inayoongoza na kuyasimamia maisha maisha yao!  Na ifahamike kuwa mwadamu huwa vile anavyojifikiria, kwa hiyo basi endapo itatokea mwan...

Hakuna Uhalisia Wowote Ule Kwenye Usemi Usemao; "Wengi Wape"

Image
Hivi unafahamu kuwa kuna mambo mengi sana ambayo yanaaminika na kundi kubwa la watu duniani kote, ya kwamba mambo hayo ni kweli na ilipaswa yawe vile yalivyo, ilihali mambo hayo siyo kweli na wala hayapo hivyo ijapokuwa yanaaminika na wengi kuwa yapo hivyo? Ukweli ni kwamba hapa duniani yapo mambo mengi sana ambayo yamepewa tafsiri fulani fulani hivi fananifu katika ulimwengu wote, kiasi kwamba yamekuwa ni ya kawaida na yamezoeleka kila mahali, na yanaaminika na wengi kuwa yapo hivyo ilihali hayapo hivyo! Huenda hata wewe ukawa ni miongoni mwa watu ambao wameamini katika mambo yasiyo na ukweli na ambayo hayawezi kuthibitishwa, hali ambayo imekufunga kifikra na kiufahamu nawe ukajikuta ukishindwa kujinasua kwa sababu umenaswa mtegoni! Rafiki, unatakiwa kujua kwamba hapa duniani hakuna kuteseka pasipo na sababu! Kwa kusema hivyo kwa kila teso unalopitia upate kujua kwamba kuna sababu inayopelekea teso hilo! Hata hivyo busara imenifundisha kwamba sina budi kutumia sikio langu ...

Hii Ni Kwa Wale Ambao Wameandaa Huduma Au bidhaa Zinazotokana Na Uwezo Wao Lakini Hawajaanza Bado...

Image
Hivi unafahamu kuwa kuna watu ambao wanatambua uwezo wao na pengine labda mara baada ya kugundua hilo, wanatoa mpaka huduma au bidhaa Fulani zinazotokana na uwezo wao lakini hawafahamiki? Unatakiwa kujua kwamba kutoa huduma fulani au kuuza bidhaa fulani siyo kigezo cha kufanikiwa katika hilo, kama hutajifunza jinsi ya kujitangaza! Ukweli ni kwamba, unatakiwa ujifunze jinsi ya kujitangaza ili uwafanye watu watambue kwamba kuna huduma au bidhaa unayoizalisha!  Rafiki, unatakiwa uwafanye watu watambue kwamba, hata wewe upo na unatoa huduma au unauza bidhaa Fulani.  Na ifahamike kwamba, kuna kundi kubwa la watu ambalo halijui chochote kile kuhusu wewe, kuhusu bidhaa zako na  kuhusu huduma yako.  Hivyo basi ni muhimu kujifunza jinsi ya kujitangaza ili uweze kuwafanya hao watu watambue uwepo wako pamoja na uwepo wa bidhaa zako na huduma yako! Na, moja ya mbinu rahisi ya kujitangaza ni kupitia kuwazoesha tu watu, kwa maana wanadamu huzoeshwa. Kwa mfano nilivyoan...