Maumivu ni Sehemu ya Safari ya Maisha
Maisha ni safari yenye milima na mabonde. Kuna nyakati za furaha na nyakati za maumivu makali ambayo kila mmoja wetu hupitia. Maumivu yapo kwenye maisha ili kukupa funzo, ili siku moja uthamini kile ambacho kiliwahi kukuumiza mara baada ya kukipata. Kwa maana fupi tunaweza kusema: kuumizwa kunaweza kuwa ufunguo wa kukupeleka kwenye furaha, kama utaruhusu maumivu yakufundishe. Lakini ieleweke vyema kwamba si kila maumivu yanakupeleka kwenye furaha. Unapaswa kujua: si kila kinachokuumiza kina thamani ya baadaye. Usijidanganye kuyatukuza yote, kwa sababu siyo yote ni ya kujenga. Kila mmoja wetu hubeba maumivu ya ndani—ya kifamilia, kikazi, kimapenzi, kifedha, kielimu, au hata ya kitaifa. Mimi ninayeandika haya pia hupitia maumivu makali nyakati fulani. Lakini ukweli ni huu: *tatizo siyo maumivu yenyewe, bali ni namna unavyoitikia.* Ukiwa kwenye kipindi kigumu, jiulize maswali haya muhimu: 1. *Chanzo chake ni nini?* – Je, ni wewe mwenyewe, mzazi, ndugu, mwenzi, au ha...