Posts

Showing posts from May, 2023

Jinsi Ya Kupata Matokeo Unayoyataka... Mbinu Ya 2&3

Image
2. Tafuta Njia Zitakazokusaidia Ili Ufanikiwe Kupata Kile Unachokitaka... Kujua unachokitaka siyo kigezo cha kukipata, bali ni lazima uweke wazi  njia zitakazokusaidia ili upate hicho unachokitaka.  Rafiki, hakuna matokeo ambayo hujitengeneza yenyewe pasipo njia zitakazochochea matokeo hayo… Na, ndiyo maana hata katika hesabu huwezi kupata jibu pasipo kutumia formula/njia fulani. Hebu jaribu tu kuvuta picha utapateje jibu (matokeo) pasipo kutumia njia fulani itakayokuletea jibu hilo (matokeo hayo)? Hii ni sawa na kusema, katika kila utakachokitaka kuna njia utakayopsawa uitumie ili ikusaidie uweze kukipata kitu hicho! Na, ndiyo maana niko hapa kukukumbusha kuwa ukishajua unachotaka lazima udokeze mbinu utakayopasawa uitumie ili ukipate! Kwa mfano katika hoja ya kwanza nilisema kwamba ninachokitaka ni “kuongeza pato langu la mwezi lifikie 300,000/=” kwa mantiki hiyo itabidi niweze kuja na njia ambazo zitanisaidia ili niweze kuyapata matokeo hayo ninayoyataka.  ...

Jinsi ya kupata matokeo unayoyataka…

Image
Hivi unafahamu kwamba asilimia kubwa ya watu hushindwa kupata matokeo mazuri juu ya kile wanachokitaka na wengine huishia kupata matokeo yaliyo kinyume kabisa hasa ukihusisha na yale matokeo wanayoyataka? Huenda na wewe umekuwa miongoni mwa watu hawa, ambao wameshindwa kupata matokeo ya kile wanachokitaka kwa asilimia zote, au wamepata kinyume chake. Unatakiwa kujua kwamba watu wengi wanajua wanachokitaka lakini hawajui jinsi ya kukipata, kutokana na hilo hujikuta wakitumia mbinu zisizokuwa sahihi katika kutafuta kile wanachokitaka mwisho wa siku wanaishia kutokupata kitu chochote kile. Mbali na hilo katika kuishi kwetu tuna lile kundi kubwa la watu ambalo lenyewe halijaweka wazi juu ya kile linachokitaka kukipata, hii inamaanisha kwamba kwa sababu hawajakusudia kitu hawawezi kupata matokeo juu ya kitu kisichokusudiwa!  Kwani katika hali ya kawaida huwezi ukakipata kitu ambacho hukitafuti hata kama kitakuwa katika mazingira uliyopo… Unatakiwa kujua kwamba ukiweka wazi k...

Jinsi Ya Kuanza Upya Tena... mbinu ya 6&7

Image
6. Badili Tabia Zako Huwezi ukapata matokeo mapya kama hutabadili tabia zako. Kwani ukiwa ni mtu wa kuendelea kufanya tabia zilezile huwezi ukapata matokeo ya tofauti na yale ambayo huwa unayapata siku zote. Unatakiwa kujua kwamba mafanikio ni kitu unachokivuta kutokana na mtu unayekuwa. Na, umekuwa hivyo kutokana na mjumuisho wa tabia zako zote uzifanyazo.  Hii inamaanisha kwamba umejitenegeneza mpaka ukawa hivyo ulivyo mbali na ukweli kwamba uliumbwa na Muumba. Kumbuka kwamba tabia zako zikishakomaa huanza kukutambulisha kwa watu, hivyo watu watakutambua wewe ni nani kutokana na tabia zako. Unatakiwa kujua kwamba hapo ulipo na hivyo ulivyo ni kwa sababu yako mwenyewe pamoja na tabia zako.  Huenda ulikuwa ni muumini wa kuweka visingizio, huenda ulikuwa ni muumini wa kughairisha mambo, huenda ulikuwa ni muumini wa kutokuwajibika ipasavyo, huenda ulikuwa ni muumini wa kulaumu na kutaka kuonewa huruma, huenda ulikuwa ni muumini wa kutumia muda wako vibaya,  huen...

Jinsi Ya Kuanza Upya Tena... Mbinu ya Tano

Image
5.Tafuta Maarifa Mapya Kila Leo...... Tunaishi kwenye dunia inayobadilika kila leo hivyo sote tunatakiwa tuwe wanafunzi kwamba tujifunze kila iitwapo leo.  Unatakiwa kujua kwamba kama hauna taarifa sahihi utapoteza uelekeo, kama haujitengenezi kuwa bora basi unazidi kuharibika.  Kama haufanyi jitihada katika kujiboresha basi utapitwa na wakati… Mifumo iliyotutengeneza kuna wakati imetufunza mambo ya kizamani kiasi kwamba mtu unahitimu hata shule ukiwa na taarifa za zamani!  Hebu vuta picha umefundishwa kupitia mtaala wa zamani, old school curriculum ni kipi kipya utakifanya kwenye dunia hii ya kisasa? Kanuni ya kitokacho na kiingiacho inasema kwamba "kitakachotokea kitakuwa sawa na kilichoingia" Hii inamaanisha kwamba utafanya mambo fulani kutegemeana na maarifa yaliyoingizwa kichwani mwako! Jaribu kufikiri tu, ni kipi utakifanya kwenye hii dunia ya kisasa ilihali kichwani mwako kuna mafaili ya zamani!  Hebu vuta picha umepewa maarifa ya dunia iliyokuwepo...

Jinsi Ya Kuanza Upya Tena... mbinu ya 3&4

Image
3.Jitambue Kwanza Wewe Ni Nani Sizungumzii kujua jinsia yako, sizungumzii kutambua jina lako, sizungumzii utambulisho unaotokana na kazi unayoifanya na wala sizungumzii utambulisho unaotokana na kozi uliyosomea!  Unatakiwa kujua kwamba kuna utambulisho wa kutengenezwa kutokana na mifumo ya nje, pamoja na utambulisho unaojitengenezea mwenyewe mara baada ya kutambua kwanini ulizaliwa na kwa nini bado uko hai! Vilevile unatakiwa kujua kwamba kujitambua ni kama kibali kitakachokuruhusu uishi maisha yenye hadhi fulani, kwamba utauishi ukuu au udhaifu  wa maisha yako kutokana na vile unavyojitambua! Na ifahamike kwamba, kujitambua wewe ni nani inaweza kuwa safari ndefu  kidogo, kwani ili  upate kujitambua itakulazimu uanze kutafuta sababu ya kuumbwa kwako pamoja na kusudi lililomfanya Mungu akuumbe!  Na, ndiyo maana moja ya tafsiri nyepesi ya kujitambua ni ile inayofafanua kujitambua kama ile hali ya mimi kufahamu sababu yangu ya kuishi pamoja na kuwepo ha...

Jinsi Ya Kuanza Upya Tena mbinu ya pili

Image
2. Rudi kwenye chanzo chako "Ee bwana umenichunguza na kunijua,  Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;   Umelifahamu wazo langu tokea mbali". Zaburi 139 "Kabla sijakuumba katika tumbo la mama yako nalikujua na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa"… “Yer 1:5”.  Nimeanza na hiyo mistari miwili ili ujue kwamba kuna yule ambaye anakujua wewe kuliko hata wewe mwenyewe unavyojijua. Kwamba ukirudi kwake ukajikabadihi naye atakuongoza na kukupeleka kule anakotaka akupeleke, kwani yeye ndiye aujuaye mwanzo na mwisho wako.  Na, ndiyo maana isaya 48:17 neno la BWANA linasema “BWANA, mkombozi wako, mtakatifu wa Israel, asema hivi, Mimi ni BWANA, MUNGU wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongazaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Unatakiwa kujua kwamba mawazo yetu pamoja njia zetu si kitu kwani huwa na ukomo, kwamba unaweza ukazifuata na usifike popote pale kwa sababu hujaanza na Mungu. Na, ndiyo maana, Isaya 55:8-9 inasema kwamba “maana mawazo yangu si ma...

Kutoka 100% Hadi 0%Jinsi Ya Kuanza Upya Tena…

Image
Hivi unafahamu kwamba karibu kila binadamu katika kuishi kwake huwa anafika hatua fulani na kuona ni bora kuanza upya kuliko kuendelea kuishi kimazoea, huku akiwa hana cha maana anachokipata kutokana na mwenendo wake wa kuishi? Huenda hata wewe hapo ukawa uliweka matarajio makubwa sana kuhusu maisha yako, kwamba ulitarajia uje uishi maisha mazuri yenye furaha, Amani pamoja na mafanikio, lakini umejikuta muda unazidi kwenda mbele na hakuna chochote kile cha maana kinachotokea maishani mwako… Nafahamu ni jinsi gani hali hii inakuumiza, kwani mbali na kufanya juhudi kubwa sana pamoja na kujitoa kwako kwa asilimia zote, mwisho wake umejikuta unaishia kuambulia patupu… Huenda ulikuwa na matarajio murua kabisa kuhusu mahusiano yako cha ajabu umejikuta upo kwenye mahusiano ambayo hata hujui yanahusiana na nini… Huenda ulikuwa na matarajio mazuri sana kuhusu kipato unachotaka kutengeneza kwa mwezi, lakini mwisho wa siku unaishia kuambulia patupu… Huenda ulikuwa una matarajio makubw...

Jinsi Watu Huitikia Kuhusu Matatizo...

Image
1. Kulidharau Hawa Ndiyo Wale Watu Huamua Kusema “Liwalo Na Liwe”, Jaribu Kufikiri Kuhusu Kitu Kinahusu Maisha Yako Halafu Unaamua Kukipuuzia Kwa Kusema Liwalo Na Liwe Vipi Kama Halitakuwa? Na Vipi Kama Litaleta Matoke Mabaya?  Unafikiri Hayo Matokeo Yatamkuta Nani Kama Siyo Wewe Mwenyewe? Unahitaji Kufikiri Juu Ya Hili… 2. Kulaumu Sasa Aliyekuambia Kulaumu Hubadili Kilichotokea Ni Nani? Hakuna Kiwango Cha Lawama Ambacho Hutatua Tatizo…  Hii Si Njia Sahihi Ya Kulikabili Tatizo Kwani, Kulaumu Ni Kitu Kingine Na Kutatua Tatizo Kingine, Acha Kulaumu Kabili Tatizo Kwa Njia Sahihi. 3. Kuwekeza Juhudi Na Nguvu Kubwa Kwenye Tatizo… Yaani Badala Ya Kuweka Juhudi Kutafuta Chanzo Cha Tatizo Wewe Unaweka Juhudi Kwenye Kukikabili Kilichotokea. Je Ni Kwamba Hautambui Kwamba Kila Matokeo Yana Kichocheo Ambacho Hupelekea Kutokea Kwake? Na, Kama Unatambua Kwanini Unahangaika Na Kilichotokea Na Siyo Kuhangaika Na Kile Kilichopelekea Kutokea Kwake? Ndugu Ili Utatue Changamoto Unatak...

Kwani Tatizo Lako Ni Nini…?

Image
Hivi Unafahamu Kuwa Asilimia Kubwa Ya Watu Duniani Kote Huishia Kulaumu Kuhusu Matatizo Wanayokumbana Nayo Pasipo Kuchukua Hatua Stahiki Dhidi Ya Matatizo Hayo? Suala Hili Ndilo Limechangia Kwa Kiasi Kubwa Dunia Iwe Ni Sehemu Ya Kukutana Na Matatizo Ya Kila Aina.  Hii Ni Kwa Sababu Watu Waliopo Wanakumbana Na Matatizo, Halafu Hawachukui Hatua Yoyote Ile Katika Kuyakabili. Kutokana Na Hilo Matatizo Hayo Yanakuwa Yanarithishwa Kizazi Hadi Kizazi... Pia, Unatakiwa Kujua Kwamba Huwezi Ukapata Matokeo Tofauti, Kama Utaendelea Kufanya Mambo Yaleyale Ambayo Umezoea Kufanya Siku Zote.  Hii Inamaanisha Kama Umekuwa Ni Mtu Wa Kulaumu Tu Kuhusu Matatizo, Endapo Hutobadili Njia Nyingine Ya Kuyakabili Matatizo Zaidi Ya Kulaumu, Huwezi Ukapata Matokeo Tofauti, Bali Matatizo Yako Yatabaki Palepale... Hata Hivyo Ni Muhimu Ukafahamu Kwamba Hakuna Kiwango Cha Lawama Ambacho Hutatua Tatizo, Laumu Utakavyoweza, Ukiweza Tukana Hata Kutukana, Lakini Nipo Hapa Kukufahimisha Kuwa Hakuna C...

Badili Fikra Zako Badili Maisha Yako...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba maisha yako yamekuwa hivyo yalivyo kutokana na fikra zako mwenyewe?  Unatakiwa kujua kwamba katika maisha huwezi ukakivuta kitu ambacho hujakitengeza kupitia fikra zako! Mbali na hilo unatakiwa kujua kwamba hata hatima ya maisha yako huanza kama fikra, yaani unapanda wazo/dhana unavuna kitendo, unapanda kitendo unavuna tabia, unapanda tabia unavuna utambulisho, unapanda utambulisho unavuna hatima ya maisha yako! Na, hivyo ndiyo mduara wa maisha yako ulivyo, kwamba  maisha yako yamekuwa hivyo kwa sababu, yalianza kutokana na dhana/mawazo uliyoyatengeza kupitia fikra zako mwenyewe.. Kutokana na ukweli huo, ndiyo maana ilishawahi kusemwa Kwamba maisha ya binadamu ni matokeo ya fikra zake mwenyewe! Hii inamaanisha kwamba, umefika hapo ulipo kimaisha na umekuwa hivyo ulivyo kutokana na fikra zako mwenyewe! Na, ndiyo maana kanuni ya kupanda na kuvuna inasema kwamba "utavuna ulichokipanda"  Kinachomaanishwa hapa...

Utabadili Maisha Yako Siku Utakayojua Wewe Ni Nani...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba zaidi ya asilimia 80 ya watu wengi hapa duniani, hawana uelewa wa kutosha kuhusu wao wenyewe kiasi kwamba hawajui wafanye nini au wajifanyie nini?  Tatizo hili limekuwa ni sugu sana, kiasi kwamba tumekuwa na watu wazima (hewa) ambao hawana mchango wowote ule katika kubadili maisha yao na hata kuibadili jamii yetu! Hali hii imepelekea maisha yetu Yazidi kudumaa na kudidimia zaidi kadri siku zinavyozidi kwenda mbele... Hata hivyo, wadau walisema kwamba, kile usichokijua ndicho kitakachokuangamiza siku moja. Hii inamaanisha kwamba usipojijua wewe ni nani, basi huko kutokujijua ndicho kitakuwa chanzo cha maangamizi yako! Mbali na hilo Neno la Mungu linasema "Watu Wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa" Kinachomaanishwa hapa ni kwamba, kama hutakuwa na maarifa ya kukutosha, basi ukosefu wa maarifa hayo ndicho kitakuwa chanzo cha maangamizi Yako!  Tupo kwenye dunia ambayo ina kizazi kilichojaa ukaidi mwingi sana!...

kila Mtu Kaumbwa Kwa kusudi Fulani

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivii   unafahamu kwamba kila mtu ameumbwa kwa ajili ya kutimiza kusudi Fulani hapa duniani? Unatakiwa kujua kwamba hujaumbwa uje uishie kuwa mzururaji au msindikizaji tu hapa duniani, bali kuna sababu iliyomfanya Mungu aachilie uumbwaji wako! Hii inamaanisha kwamba, hiyo sababu ilikuyokuwepo nyuma ya pazia iliyopelekea kuumbwa kwako, ndiyo ilibeba kusudi halisi la wewe na maisha yako!  Vilevile unatakiwa kujua kwamba pasipo kujua kusudi lako hutouishi ukuu wako, bali utaishia kuwa mtu wa kawaida tu, ilihali umebeba kusudi lisilo la kawaida kabisa ndani Yako!  Hivyo basi, kutokana na ukweli huo unatakiwa kujua kwamba, hukuumbwa kwa bahati mbaya, bali uliumbwa ili uje uwe mtu mkuu na mtatua matatizo ya watu!  Kamwe usimlaumu Mwenyezi Mungu kwa kuumba (huenda ukawa unapitia magumu na mateso mengi sana hivyo unaamua kuachilia lawama), bali jilaumu mwenyewe kwa kutokutafuta na kugundua kusudi la kuumbwa kwako! Unatakiwa kujua kw...