Posts

Showing posts from August, 2023

Huwezi Kuishinda Hofu Mpaka Usome Kwanza Hii...

Image
Habari yako rafiki? Ni matumaini yangu u mzima wa afya! Ashukuriwe Mungu kwa neema zake nyingi! Hatimaye leo hii somo letu la Mbinu tisa za kuikabili hofu linaenda kutamatika kwa kuangazia hoja tatu zizokuwa zimebaki! Karibu uweze kupata mbinu hizi tatu za mwisho zikusaidie katika Kuikabili Hofu...  7. Badilisha Mitizamo Yako… Siyo kila anayeona, anaona, na siye kila anayesikia, anasikia.  Kuna wengine wanaona lakini ni vipofu, na kuna wengine wanasikia lakini ni viziwi. Ninasema hivi kwa sababu watu wengi huwa hatuoni vitu kwa namna ile inavyopaswa iwe, bali tunaona vitu kutegemeana na sisi tulivyo… Ukweli ni kwamba tupo watu wengi ambao tunaona mambo kwa kulinganisha na jinsi sisi wenyewe tulivyo, kutokana na hilo tutajikuta tukijitengnezea milima na mwisho wa siku tunaanza kuhofia mambo hayo!  Mwanzo 1:26 Neno la Mungu linasema; Mungu akasema, “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu”… Chukua neno “kwa mfano wetu”, halafu weka akilini mwako!  Iko ...

Je Unataka Kujua Mbinu Za Kuikabili Hofu? Hizi Hapa Usome Halafu Uzitumie...

Image
  Habari yako rafiki? Ni matumaini yangu u mzima wa afya! Ahsante sana kwa uvumilivu wako na utulivu wako ambao umekuwa nao ukisubiri mwendelezo wa somo hili!  Huu ni wakati muafaka wa kuendelea na somo letu linaloangazia kuhusu mbinu tisa za kuikabili hofu... Awali nilidokeza mbinu mbili unazoweza kutumia kukabili hofu yoyote ile! Ashukuriwe Mungu kwa neema zake nyingi, kwa maana unaenda kujifunza mbinu nyingine nne za kuikabili hofu kama ifuatavyo:- 3. Tafuta Maarifa Mapya Kila Leo… Hosea 4:6 “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umekataa maarifa, mimi nami nitakutakataa wewe…” Friend kama hakuna kuduwaa pasipo sababu, basi hakuna hofu pasipo kuwepo kwa sababu inayopelekea hofu hiyo…  Moja ya sababu ambayo huwafanya watu wengi wahofu ni kukosa maarifa pamoja na maandalizi ya kutosha hasahasa kwenye maeneo ambayo wanaenda kukabiliana nayo.  Na, ifahamike kwamba endapo utakosa maarifa juu ya maeneo hayo kitakachofuatia hapo huwa ni a...

Fahamu Kuhusu Mbinu Ya Pili Ya Kuikabili Hofu...

Image
Hello habari yako rafiki? Ni matumaini yangu u mzima wa afya!  Karibu kwenye mwendelezo wa somo linaloangazia kuhusu mbinu tisa za kutumia ili uikabili hofu! Kwa leo umesogeweza mbinu ya pili unayoweza kutumia ili uikabili hofu!  Ikumbukwe makala iliyopita ilidokeza hoja moja! Bila kukupotezea muda ngoja nikuoneshe mbinu ya pili unayoweza kutumia ili uikabili hofu... 2. Tumia Conscious Mind Na Subconscious Mind... Unamiliki akili moja ambayo hufanya kazi kwa kutumia sehemu mbili za akili ambazo ni: conscious mind (akili dhamiri) pamoja na subconscious mind (sehemu ya akili usiyo na mamlaka nayo). Nini Maana Ya Conscious Mind? Conscious mind, ni sehemu ya akili ambayo huchukua wazo, taarifa, hisia au dhana ya kitu chochote kile na kisha kukipeleka ubongoni. Sehemu hii ya akili ndiyo huongoza maisha ya binadamu na hii ni kutokana na sehemu hii ya akili kuwa na uwezo wa kudadisi pamoja na kuchagua vitu mbalimbali kuhusu machaguo ayafanyayo huyo binadamu.  Jambo m...

Huwezi Ukafahamu Madhara Ya Kuendekeza Hofu Mpaka Usome Kwanza Hii...

Image
Hakuna kitu ambacho hufanyika kisicholeta matokeo fulani! Unachopaswa kujua ni kwamba, kwa chochote kile unachokifanya ni lazima kitaleta matokeo fulani maishani mwako! Na ifahamike kwamba, matokeo hayo huwa ya aina mbili, aidha matokeo mazuri au mabaya. Yafuatayo ni matokeo ya kuendekeza hofu: 1. Utampoteza Mungu Katika Maisha Yako… Mtu ambaye ana hofu cha kwanza haamini katika Mungu, kwa maana kila jambo linawezekana kwake yeye aaminiye.  Hivyo basi pasipo kujua hofu humuondoa kwenye chanzo chake na kumfanya aendelee kutapatapa. Ukweli ni kwamba Mungu hashindwi na chochote kile, kwake yeye kila jambo linawezekana… Hivyo basi kwa yule mtu ambaye ana hofu ni rahisi sana kumpoteza Mungu kwa maana anakuwa hana tumaini…  Na ukishampoteza Mungu maana yake utakuwa unaongozwa na akili zako pamoja na kutumainia njia zako ambazo mwisho wa siku zitakupeleka mautini… Mithali 14:12 neno la BWANA linasema; “iko njia ionekanayo sawa machoni pa mtu, lakini mwisho wake njia za ma...

Njia kuu tisa za kuikabili hofu yoyote ile...

Image
Kwa kila hali au tatizo lolote lile lililo katika maisha yako, linakuhitaji wewe mwenyewe uchukue hatua katika kulikabili au kulitatua! Na endapo hautachukua hatua katika kulitatua, hakuna atakayechukua hatua kwa niaba yako. Kumbuka mambo yaliyotulia yatabaki katika hali ile ile ya utulivu mpaka pale yatakapobadilishwa. Je, umekuwa ukihofu kwa muda mrefu sana maishani mwako?  Kama jibu ni ndiyo basi ndani ya sekunde chache zijazo unaenda kubadili kabisa historia ya maisha yako... Na, endapo utafuata kilichoandikwa katika makala hii hatua kwa hatua, nakuhakikishia hutoogopa chochote kile isipokuwa hofu ndiyo itaanza kukuhofia wewe... Je nifanye nini niikabili hofu? Usijalii fanya yafuatayo:-  1. Rejesha Imani Kwa Mungu Wako…             Zaburi 34:4 “Nalimtafuta BWANA akanijibu, akaniponya na hofu zangu zote” Mpenzi ni mara ngapi umelia na Mungu kuhusu hofu zako au hata hujawahi kabisa kumueleza?  Daudi anakuhabarisha kwamba umtafut...

je Umekuwa Ukikumbwa Na Hofu Maishani Mwako? Hizi Hapa Ndizo Sababu Ambazo Hupelekea Hofu... Sehemu ya pili...

Image
Makala iliyopita ilidokeza hoja tano kuhusu sababu za hofu! Makala hii ni mwendelezo wa makala iliyopita... Kwa leo nitadokeza hoja nyingine tano zinazodokeza sababu za watu kuhofu! Karibu sana ufuatilie makala hii... 6. Kukosa Imani Na Mungu… Watu wengi wanamwabudu Mungu lakini ni watu wachache sana wanamwamini Mungu kwamba anaweza akatenda.  Sasa kama kwake Mungu kila jambo lawezekana ni kipi kitakuwa dhidi yako kikutie hofu endapo utamwamini yule wa yawezekanayo? Mtu ambaye ana hofu kuna wakati anakuwa amekosa Imani na Mungu akaamua kutumainia akili zake pamoja na njia zake zenye ukomo, mwisho wa siku yanamshinda anaanza kuhofu na kujihisi mnyonge. Mithali 3:5-6 Neno la Bwana linasema, “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako mkiri yeye, naye atanyoosha mapito yako” Friend mpe Mungu nafasi katika maisha yako, ndiyo maana unafundishwa uenende kwa imani na siyo kwa kuona kwa maana ukienda kwa kuona utaanza kuhofia. Kun...