Posts

Showing posts from December, 2024

Usimtendee Mwenzio Yale Ambayo Haupo Tayari Kutendewa... The Golden rule

Image
Hivi unafahamu kwamba Moja ya sababu kubwa ambayo imesababisha magumu mengi tunayopitia wanadamu wengi katika nyakati hizi ni kukosekana kwa upendo baina yetu? Laiti kama kila mtu kwa kadri ya jinsia yake angekuwa anamtendea mwenzake yale ambayo hata yeye mwenyewe yupo tayari kutendewa basi hapa duniani ingekuwa ni sehemu salama sana wala kusingekuwa na chuki, hasira, vinyongo pamoja na visirani. Lakini kutokana na kukosena kwa utu na upendo baina yetu ndiyo maana chuki, vinyongo, visirani vimetapakaa sana katika kizazi hiki cha leo. Ukichimba kwa undani utagundua kuwa leo hii wapo majirani ambao hawazungumzi kutokana na chuki, wapo wamafamilia ambao hawana upendo baina yao kutokana na chuki, wapo wanandoa ambao chuki ndiyo imechukua nafasi kubwa zaidi katika maisha yao kana kwamba walioana ili wachukiane na siyo wapendane... Ukweli ni kwamba, haya yote yanatokea kwa sababu tunawatendea wenzetu yale ambayo sisi wenyewe hatupo tayari kutendewa. Hebu jaribu kuvuta picha, unam...

Je, Unataka Ubadili Fikra Zako Ili Ubadili Maisha Yako? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii..

Image
Hivi unafahamu kwamba maisha yako yamekuwa hivyo yalivyo na yamefika hapo yalipo kutokana na fikra zako mwenyewe?  Unatakiwa kujua kwamba katika maisha huwezi ukakivuta kitu ambacho hujakitengeza kupitia fikra zako! Ukweli ni kwamba hata hatima za maisha yetu huanza kama fikra, ya kwamba, unapanda wazo/dhana unavuna kitendo, unapanda kitendo unavuna tabia, unapanda tabia unavuna utambulisho, unapanda utambulisho unavuna hatima ya maisha yako! Ndugu, hivyo ndiyo mduara wa maisha yako ulivyo, kwa kusema hivyo maisha yako yamekuwa hivyo kwa sababu, yalianza kutokana na dhana/mawazo uliyoyatengeza kupitia fikra zako mwenyewe... Kutokana na ukweli huo, ndiyo maana ilishawahi kusemwa Kwamba, maisha ya binadamu ni matokeo ya fikra zake mwenyewe! Hii inamaanisha kwamba, umefika hapo ulipo kimaisha na umekuwa hivyo ulivyo kutokana na fikra zako mwenyewe! Na utakuwa huyu ama yule kesho yako endapo utaamua kubadilisha fikra zako! Unatakiwa kujua kwamba fikra zako ni kama mbegu ina...

Je, Nitajuaje Kama Hili Ndilo Kusudi Langu?

Image
Ni ngumu sana kuweza kulibaini kusudi lako ilihali tayari kuna kusudi dogo ambalo unaliishi.  Tupo watu wengi sana ambao tumeridhika na kazi tunazozifanya kwa sababu tunatengeneza fedha na tumeshapata tayari uwezekano wa kuishi.   Kutokana na hilo wengi wetu tumeishia kuona ndivyo maisha yetu yalivyopaswa yawe.  Hii ni mbaya sana, awali nilisema kwamba kufanya kazi Fulani siyo kigezo cha wewe kuliishi kusudi lako.  Hata mimi ninayeandika makala hii ni mwalimu mtaalamu na nina shahada ya kwanza ya sanaa na elimu.  Na hata sasa ninafanya kazi kama mwalimu. Lakini kwanini ninafanya uandishi, ni kwa sababu huku ndiko najisikia fahari zaidi, na ninaona kabisa maisha yangu yalitakiwa yawe hivi. Kwa hivyo hata mimi ninaweza kusema ni mtu ambaye ninakiishi kile ambacho niliumbwa nikiishi, kwa sababu ni kitu ambacho nilikuwa nikipatwa msukumo wa kukifanya.  Je, unataka kujua kusudi huwa lina sifa gani? kama jibu lako ndiyo soma sifa zifuatazo:- 1. ...

Jinsi Ya Kuwa Mtu Usiyesimamishwa Na Chochote Kile..

Image
Mbinu Ya Saba Bobea Katika Eneo Fulani Vile unavyokuwa unajua kuhusu jambo Fulani kwa undani  ndivyo unavyopata ujasiri na utayari wa kufanya jambo hilo.  Kwa kusema hivyo, unapobobea katika eneo Fulani inamaanisha kwamba, utakuwa ni yule mtu ambaye huwezi ukasimamishwa kwa sababu tayari una ubobevu wa kutosha na unalijua eneo hilo kiundani. Ndugu unatakiwa kujua kwamba hakuna nyota wa eneo zaidi ya moja, kwa sababu kila nyota huamua kubobea katika eneo moja ili adhihirishe uwezo wake.  Ndivyo unavyopaswa kufanya kwa kuchagua eneo moja kisha lichimbue kiundani ili upate uelewa ulio mpana kuhusu eneo hilo!  Baada yaa hapo dhihirisha ukomavu wako na uelewa wako katika eneo hilo ama hakika hakuna kitakachokusimamisha!  Kwa mfano mbali na kugundua kuwa nina uwezo wa kuandika, sikuanza tu kuandika moja kwa Moja! Niliamua nijifunze kwanza kozi ya uandishi ili niweze kuandika vizuri, nilitambua fika kabisa ya kuwa, kipaji pekee huwa hakitoshi, kwa sababu ut...

Jinsi Maendeleo Ya Sayansi Na Teknolojia Yamesababisha Watu Wajione Vile Wanavyojiona...

Image
Angalizo: sipingani na maendeleo ya sayansi na teknolojia wala sitaki mtu apuuze haya maendeleo kwani yamerahisisha maisha, lakini ninaibua hoja inayoonesha ni kwa namna gani maendeleo ya sayansi na teknolojia yameathiri watu kimtizamo yaani vile wanavyojiona na ifahamike kwamba kila chenye faida huwa hakikosi kuwa na hasara!  Tafadhali elewa nazungumzia ni kwa namna gani sayansi na teknolojia imesababisha watu wajione vile wanavyojiona!  Kwanini nasema sayansi na teknolojia imebadilisha watu kimtizamo? Sababu kubwa inayonisukuma niseme ni kwamba watu wengi wamejikuta wakitumia sayansi na teknolojia kama kioo cha kujitazamia!  Matokeo yake wameishi kujiona wao ni wabaya kimuonekano (hasa wakihusisha rangi zao pamoja na muonekano wa maumbile yao).  Kutokana na hilo wakaanza kujishushia hadhi kwa kujiona wao kama siyo kitu, pasi na kujua kwamba kioo walichotumia kujitizamia siyo kioo halisi!  Kwa mfano maendeleo ya sayansi na teknolojia yamekuja na ug...

Je, Unataka Kujua Sifa Pambanuzi Za Kusudi? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii...

Image
2. Kusudi Ni Jambo Linaloendana Na Wewe Ulivyo Upo hivyo ulivyo kwa sababu upo hivyo. Na upo hivyo ulivyo ili uweze kuliishi kusudi lako! Umeumbwa na rangi hiyo uliyonayo kwa sababu kuna kusudi la uwepo wa rangi hiyo maishani mwako.  Umeumbwa na huo mwili ulionao kwa sababu kuna kusudi la wewe kuumbwa hivyo. Katika hali ya kawaida hata mionekano ya vitu alivyovitengeneza mwanadamu hupima kusudi la vitu hivyo.  Kwa mfano vile gari la kuchukua mchanga lilivyo ni tofauti kabisa na vile gari la kuchukua abiria lilivyo kimuonekano. Vile ndege ilivyo ni tofauti kabisa na meli ilivyo. Kwa kusema hivyo, ndege imetengenezwa kwa kusudi la kuweza kupaa, ilihali meli imetengenezwa ikiwa na uwezo wa kuelea juu ya maji.  Na aliyetengeza ndege, aliiunda kwa kulinganisha na vile ndege asilia walivyo. Huku hata aliyejenga meli alijenga sawa na na vile samaki walivyo kwa sababu wana uwezo wa kuelea juu ya maji. Kwa hivyo hata wewe upo hivyo ulivyo, ukiwa na mwili huo ulionao, ...

Je, Unataka Kujua Kwanini Baadhi Ya Watu Hushindwa kugundua Kusudi la Kuumbwa Kwao? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii...

Image
Kanuni ya matokeo na kichocheo inasema; “Kila kitu hutokea kutokana na sababu na hakuna kitu ambacho hutokea pasipo na kisababishi ambacho huchochea katika kutokea kwake.”  Na kama uhalisia uko hivyo inaamanisha kwamba zipo sababu nyingi sana ambazo husababisha baadhi ya watu washindwe kugundua kusudi la kuumbwa kwao!  Hata hivyo zifuatazo ni sababu hizo, fuatana nami kwa madaha tukazitalii sababu hizi kwa kina!  1. Kutokuwa Na Mahusiano Mazuri Na Mungu  Anayetambua matumizi sahihi ya kifaa Fulani ni mtengenezaji, na kifaa hicho hakiwezi kutambua kilitengenezwa kije kitumike kwa ajili gani kama hakitapokea maelekezo kupitia aliyekitengeneza. Na kama iko hivyo kinaweza kikabatilishwa hata matumizi yake kwa sababu hakijapata maelekezo kutoka kwa mtengenezaji wake juu ya namna gani kinaweza kikatumika. Na ndivyo ambavyo wengi wetu tumebatilisha/tumebetilishwa namna tulivyopaswa tuje tutumike hapa duniani kwa sababu ya kutokuwa karibu na chanzo cha uhai wetu ...

Kama Una Roho Nyepesi Tafadhali Usisome Ujumbe Huu…

Image
Ila Hapa Duniani Kuna Watu Ni Ving’ang’anizi... Ndugu, Si Umeshatahadharishwa Kwamba Usisome Lakini? Ama Hakika Unachokitafuta Utakipata... Je, Una Roho Ngumu Kiasi Kwamba, Utaweza Kuyakabili Mambo Mazito Yatakayojadiliwa Humu? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Basi Songa Nayo…  Hivi Unafahamu Kuwa Hapa Duniani Tunaishi Watu Wenye Matabaka Mawili Tofauti, Ambao Ni: Watawala Na Watawaliwa? Na Katika Haya Makundi Mawili Watawala Ni Wachache Huku Wanaotawaliwa Wakiwa Ndiyo Wengi Zaidi? Huenda Hata Wewe Ukawa Unatawaliwa Na Hujui, Leo Nipo Hapa Kukusanua Kwa Kukuletea Ukweli Unaopaswa Kuujua, Lakini Sikuamuru Ufanye Nini Kwa Sababu Wajibu Wangu Mimi Ni Kukuonesha Tu! Nawe Utachukua Hatua Ikiwa Utakuwa Na Nia Thabiti Ya Kubadilisha Maisha Yako! Mara Zote, Tabaka Tawala Huweza Kuanzisha Mifumo Fulani Hivi Ambayo Wale Wanaotawaliwa Wasipotizama Kwa Undani Huona Kana Kwamba Wananufaika Nayo, Ilihali Mifumo Hiyo Imetengenezezwa Ili Iwanyonye Pamoja Na Kuwazuia Wasiuishi Uwezo Wao Na Mao...

Kama Hujui Kusudi Lako, Hujui Maana Ya Maisha Yako...

Image
Mbali na kuwa kila mwanadamu ana uhuru wa kuishi hapa duniani pasipo bugudhi wala usumbufu, kuna wakati ukifika, uhuru huo hugeuka na kuwa uchungu na majuto makubwa sana, hasa pale inapotokea mtu huyo akashindwa kujua kwanini anaishi na kwanini maisha yake yapo… Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika, zimeonesha kwamba wapo watu wengi sana ambao wanaishi huku wakiwa wamechanganyikiwa maishani mwao kwa sababu hawana majibu sahihi juu ya maswali mbalimbali ambayo daima hujiuliza, na mara nyingi maswali hayo huwa yamelenga zaidi katika kuhoji kwanini maisha yao yapo.  Ukweli ni kwamba, katika ulimwengu huu ulio mpana sana, karibu kila mtu aliye hai huwa anajikuta akijihoji juu ya maswali yafuatayo; “Hivi mimi ni nani”, “Kwanini nilizaliwa” na “Kwanini ninaishi.”  Mbali na kuwa wengi wao hujiuliza maswali kama hayo, huishia kutopata majibu muafaka, matokeo yake hubaki wakiwa hawajui wafanye nini na maisha yao!  Bila shaka hata wewe ulishawahi kujiuliza maswali kama ha...

Je, Unataka Kujua Kusudi Ni Nini? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii..

Image
Kwa tafsiri nyepesi neno Kusudi linaweza kufafanuliwa kama kitendo cha kutekeleza mpango wa Mungu kukuumba hapa duniani!  Au, Kusudi ni kufanyika kwa jambo Fulani. Hii ni sawa na kusema kwamba, kuna kusudi lililopo kutokana na kufanyika kwa maisha yako hapa duniani.  Ukweli ni kwamba kila mtu kaumbwa kwa kusudi Fulani, lakini kutokujua kusudi la kuumbwa kwako isiwe sababu ya kukufanya, useme ya kuwa ulipaswa uwe hivyo ulivyo sasa.  Rafiki unatakiwa kujua kwamba, ujinga wa kutokujua kusudi la uwepo wa kitu Fulani hauondoi kusudi la kitu hicho. Kwa kusema hivyo kusudi la kitu hicho litabaki kama lilivyo. Kwa maneno mengine ni sawa na kusema, kama vile mtu aliyetengeneza dawa alivyotambua kusudi la kutengeneza dawa yaani matumizi yake ambayo ni kutibu ugonjwa, vilevile hata Mungu alikuwa na kusudi la kukuumba hapa duniani. Hata ukienda kusoma maandiko matakatifu utagundua kwamba, Mungu huwa ana kusudi la kumuumba kila mwanadamu.  Tunajifunza kupitia kitabu c...

Je, Kazi Yangu Ndiyo Kusudi Langu? Kama Jibu Ni Hapana, Je, Kazi Yangu Ni Nini?...

Image
Hivi unafahamu kuwa watu wengi wanafanya kazi ambazo zipo nje na kusudi la kuumbwa kwao?  Ukweli ni kwamba, upo uwezekano mkubwa sana wa kazi yako kutokuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Kusudi lako!  Na endapo ikatokea kazi yako ikawa ipo nje na kusudi lako, hilo halitakuwa kusudi la kuumbwa kwako, bali ni utakuwa ni mfumo uliotengenezewa ili ukusaidie kutengeneza kipato kwa mateso na msumbufu mengi hapa duniani! Upate kujua kwamba,  Kazi ni shughuli yoyote ile iliyo halali aifanyayo mtu ili kujitengenezea kipato. Hata hivyo wafanyakazi wengi huwa ni wabobevu na wana uelewa mpana kuhusu shuguli hizo. Aidha, wengi wao huwa wameajiriwa na huwa na vyeti vya kitaaluma. Na elimu ndiyo hutumika kama kibali cha kuwaidhinisha kuwa wanastahili kufanya kazi hizo. Mbali na hilo hata kiwango cha mshahara hutegemeana na kiwango cha elimu alichonacho mtu huyo! Kwa mfano, mtu ambaye hajasoma huweza kufanya kazi za kutumia Nguvu (vibarua) na malipo yake huwa ni kidogo... Uk...

Je, Unataka 2025 Uwekeze Katika Afya Yako? Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii..

Image
Niliposoma KITABU cha "The Diary Of A CEO, The 33 Laws Of Business And Life" Katika kanuni ya tisa amesema; "Always prioritise your first foundation " Akimaanisha kwamba, huna budi kuweka kipaumbele kwenye afya yako kwa sababu huo ndiyo msingi wa maisha yako... Na unatakiwa ujenge afya yako ili uishi muda mrefu huku ukifurahia maisha. Mwandishi huyu amenukuu maneno ya Warren Buffett tajiri mkubwa sana hapa duniani katika nyakati hizi ambaye alisema; "Nilipokuwa na umri wa miaka 16 vipaumbele vyangu vilikuwa ni wanawake na magari. Sikuwa na bahati kwa wanawake lakini nilikuwa na bahati kwa magari" Huyu mwamba anadai kwamba, alitumia 80% ya maisha yake kwenye kazi, wanawake, marafiki, familia na katika kumiliki mali nyingine nyingi." Lakini alipofikisha miaka 27 mambo yalibadilika kutokana na janga la COVID-19 lililoua zaidi ya watu milioni sita. Baada ya ripoti iliyohusisha wagonjwa 400,000 kuonesha kwamba asilimia 113 ya watu wenye vitambi...

Je, Unataka Ufahamu Afya Hutengenezwaje? Kama jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii...

Image
Hivi unafahamu kwamba afya huanza kutengenezwa mara tu mimba inapotungwa? Ijapokuwa, huwa unakuwa kimwili kutokana na kile unachokula, lakini afya yako ilianza kutengenezwa tokea siku mimba yako ilipotungwa... Kwa maana Hiyo, mtindo wa maisha ya mama pamoja na mazingira yaliyopolekea ujauzito ndiyo hupima afya ya mtoto akiwa tumboni... Kwa mfano Ni juzi tu hapo watu wamefanya miruko wakiwa wanaadhimisha brithday ya Yesu, wakashindwa kufanya yaliyo ya Kiyesu. Nasikia guest na Lodge zilijaa haha utani kidogo ila usicheke, ona sasa unacheka... kwa hiyo basi kama kuna mwanamke hakujipanga akafanya miruko na mwanaume pasi maandalizi ya msingi ya kulea mimba kwa utaratibu unaotakiwa, halafu akaendelea na mtindo mbovu wa kuishi huku akiwa mjamzito, kuna uwezekano wa kuja kuzaa mtoto mwenye tatizo la kiafya... Si hao waliofanya miruko tu, pia wapo hata wanandoa ambao hawana taarifa sahihi juu ya kipi kinatakiwa kifanyike pindi mama akiwa mjamzito... Wengi hawajui mama anashauriwa a...