Posts

Showing posts from September, 2024

Hii Ni Kwa Wale Watu Wanaotaka Kubadili Maisha Yao Lakini Hawajaanza Bado…

Image
Hivi unajua kwamba zaidi ya asilimia 80 ya watanzania wanapambana sana katika kubadili maisha yao lakini jitihada zao zinagonga mwamba na kujikuta wakishindwa kupiga hatua kimaisha?  Hili ndilo tatizo unalokumbana nalo, kwa maana mbali na kupambana sana huoni matunda yanayotokana na juhudi zako unazozifanya…  Yamkini umeajiriwa aidha kwenye taasisi binafsi au serikalini lakini kila ukipokea mshahara wako unaishia kutumika wote.  Matokeo yake unabakia kapuku na madeni juu, na huna chanzo kingine cha kukutengenezea mapato, na hata ukijaribu kuweka akiba kidogo kidogo inashindikana kwa sababu kipato chako ni cha chini… Na pengine labda unatamani sana ungebadilisha hata kazi au ungeongezewa mshahara, lakini kila kunapokucha ni afadhali ya jana. Na ndiyo kwanza mambo yanazidi kuwa magumu…  Yamkini umefungua hadi biashara yako ili ujikwamue kiuchumi cha ajabu huoni maendeleo yoyote yale mbali na kuwa unafanya mauzo!  Huenda ukawa unapitia manyanyaso, dhara...

Unaweza kuwa Yeyote Yule...

Image
Dunia ni wewe unachotaka kuwa, na asili ya Dunia huwa haimfungi mtu, badala yake sasa mtu huyo anaweza akajifunga mwenyewe kutokana na mawazo yake kwa kujiwekea ukomo juu ya pale anapoweza kufika kimaisha! Na ifahamike kwamba, duniani hakuna vikwazo halisi zaidi ya vile vikwazo unavyojiwekea mwenyewe kutokana na mtindo wako wa kufikiri!  Kwa kusema hivyo umekuwa hivyo ulivyo, kwa sababu ndivyo ulivyotaka uwe, na kama hukuamua uwe hivyo inamaanisha kwamba kuna mifumo iliyokuamlia kwa kuwa hukuwa na chaguo jingine... Kwa hiyo basi, endapo utaamua, unaweza kuwa yeyote yule na hakuna mtu wa kukuzuia. Ukweli ni kwamba, hakuna cha kukuzuia wala kukusimamisha, bali ni wewe mwenyewe unaweza ukajisimamisha! Rafiki, dunia ni mali yako, kuwa unachotaka! Hutakiwi kufungwa na utambulisho wa kutengenezewa tena, badala yake sasa unaweza ukajitengenezea utambulisho wako mwenyewe, na kuwa yule unayetaka uwe... Leo hii huenda ukawa unatambulika kwa sababu ya kozi uliyosomea au kwa sababu...

Fahamu Kuhusu Athari Wanazopitia Wanawake Wanaoishi Bila Maono Maishani Mwao...

Image
Hakuna jambo lolote lile ambalo hufanyika lisilokuwa na matokeo.  Na ndiyo maana kanuni ya matokeo na kichocheo inasema; “kila kitu hutokea kutokana na sababu”. Ikimaanisha kwamba kuna Sababu za kila matokeo na hakuna kitu ambacho hutokea chenyewe bila sababu inayosababisha kutokea kwake! Kwa mantiki hiyo kumbe kuna sababu ambazo hupelekea wanawake hawa wapitie hali ngumu. Unatakiwa kujua kuwa wanawake hawa wanapitia hali ngumu si kwa sababu wanatakiwa wapitie hali hizo, bali wanapitia hali ngumu kwa sababu kuna sababu zinazopelekea wapitie hali hizo.  Ukweli ni kwamba wanawake wengi wanalaumu na kuhuzunika kuhusu mateso, taabu, manyanyaso na dharau wanazopitia lakini hakuna anayehoji kwanini anapitia hali hizo.  Kumbe sababu kubwa inayopelekea haya yote ni kuishi pasipo maono.  Je, ni nini athari za kuishi bila maono? Fuatana nami katika makala hii ufahamu athari hizo kwa maana zimechambuliwa kwa undani. Zifuatazo ni athari hizo:-  1. Kuzalishwa Na ...

Hii Ni Kwa Wanawake Tu, Fahamu Kuhusu Maeneo Muhimu Ambayo Unatakiwa Uyatengenezee Maono...

Image
Ilishawahi kusemwa kwamba wakati mzuri wa kuitabiri kesho yako ni kuiandaa leo yako.  Hata hivyo hakuna kesho mbaya kwa mtu mwenye maono mazuri kuhusu hiyo kesho , kwa sababu kile atakachokiona ndicho atakachokuja kukipata kama uhalisia wake! Mbali na kuwa wanawake wote hawafanani, hawana ndoto sawa, hawana matamanio sawa, hawaoni mambo kwa namna moja lakini kuna baadhi ya mambo ambayo ni ya kawaida kwa maisha ya kila mwanamke.  Mambo hayo ndiyo kila mwanamke anatakiwa ayatengenezee maono. Hata hivyo yapo mambo mengi sana ambayo kila mwanamke anatakiwa kuyawekea maono, lakini kutokana na uhaba wa nafasi nitajadili mambo Matano tu.  Kwa kusema hivyo huna budi kuhakikisha kuwa unatengeneza maono yako kwenye mambo haya kama kweli una ndoto za kuishi kesho iliyo njema na yenye kuvutia.  1. Maono Kuhusu Mahusiano, Ndoa Na Familia. Kila mwanamke mwenye ndoto ya kuja kuolewa huna budi kuhakikisha kuwa unatengeneza maono juu ya familia ya ndoto zako, labda uwe um...

Jinsi Ambavyo Tamaa Huwafanya Wanaume Waendekeze Ngono...

Image
Kuwa mwanaume haina maana kwamba umtamani kila mwanamke unayemuona, ni kweli kutamani kupo sikatai, Lakini kutaka kummiliki kila mwanamke unayemtamani ndipo utata unapoanzia! Cha kustaajabisha ni kwamba kuna baadhi ya wanaume ambao huwa wanaendekeza  tamaa kiasi kwamba hutaka kummiliki kila mwanamke wanayemtamani! Na ndiyo maana hata wakiwa barabarani, kazini, ofisini, mtaani ama popote pale watakapokuwepo, basi wanaume hao huwa macho juujuu kutazama wanawake wanaopita maeneo hayo.  Hali hii hupelekea hata wengine kupata ajali kutokana na kuweka umakini wao wote kuangalia wanawake na siyo kuweka umakini wote kwenye kile wanachokifanya! Hili ni jambo la ukweli kabisa wala si uzushi, huenda labda kutokana na hilo ndiyo maana wanawake nao wamekuja na staili mpya ya kuvaa nguo zinazowachora miili yao yote ili kuwatega wanaume, wameamua hata kutumia njia mbalimbali kama vile, vidonge, surgery n.k, ili kujaza nyonga na maumbile yao lengo likiwa ni kuwanasa wanaume na wen...

Nguvu Inayomilikiwa Na Mwanamke Mwenye Maono...

Image
Kila mwanamke anamiliki nguvu kubwa sana katika maisha yake lakini yule aliye na maono, ndiye mwenye uwezo wa kutumia nguvu hizo ili apige hatua kimaisha! Na hii ndiyo sababu kubwa ambayo hupelekea baadhi ya wanawake wafanikiwe kimaisha huku wengine wakibaki nyuma kimaendeleo au wakipiga hatua ndogo...  Na ifahamike kwamba, unapoishi bila kuwa na maono maishani mwako, maana yake hata nguvu zako hazitakuwa na msaada wowote ule, si hivyo tu, pia, hata rasilimali mbalimbali zinazokuzunguka hazitakuwa na maana yoyote ile kwako, kwa sababu kwenye fahamu zako hauna maono juu ya namna gani unaweza ukatumia rasilimali hizo ili ujikwamue kimaisha!  Unatakiwa kujua kwamba, maono ni picha kamili ya maisha yajayo ya mtu fulani iliyopo akilini mwake! Mara nyingi picha hizo humuonesha vile huyo mtu atakavyokuwa miaka ya mbeleni... Hata hivyo huenda ukawa unajiuliza hizo picha zinatokeaje na zinahusu nini?  Ukweli ni kwamba hizo picha hutengenezwa na mtu ambaye amejizatiti k...

Nguvu Inayomilikiwa Na Mwanamke Mwenye Maono...

Image
Kila mwanamke anamiliki nguvu kubwa sana katika maisha yake lakini yule aliye na maono, ndiye mwenye uwezo wa kutumia nguvu hizo ili apige hatua kimaisha! Na hii ndiyo sababu kubwa ambayo hupelekea baadhi ya wanawake wafanikiwe kimaisha huku wengine wakibaki nyuma kimaendeleo au wakipiga hatua ndogo...  Na ifahamike kwamba, unapoishi bila kuwa na maono maishani mwako, maana yake hata nguvu zako hazitakuwa na msaada wowote ule, si hivyo tu, pia, hata rasilimali mbalimbali zinazokuzunguka hazitakuwa na maana yoyote ile kwako, kwa sababu kwenye fahamu zako hauna maono juu ya namna gani unaweza ukatumia rasilimali hizo ili ujikwamue kimaisha!  Unatakiwa kujua kwamba, maono ni picha kamili ya maisha yajayo ya mtu fulani iliyopo akilini mwake! Mara nyingi picha hizo humuonesha vile huyo mtu atakavyokuwa miaka ya mbeleni... Hata hivyo huenda ukawa unajiuliza hizo picha zinatokeaje na zinahusu nini?  Ukweli ni kwamba hizo picha hutengenezwa na mtu ambaye amejizatiti k...