Posts

Showing posts from June, 2023

Fahamu Jinsi Maendeleo Ya Sayansi Na Teknolojia Yalivyoathiri Namna Watu Wengi Wavyojiona...

Image
Hivi unafahamu kwamba maendeleo ya sayansi na teknolojia yameleta athari nyingi zaidi kuliko faida miongoni mwa watu wengi hasa linapokuja suala la namna wanavyojiona? Unachopaswa kujua ni kwamba kila kilicho na faida hakikosi hasara! Kutokana na ukweli huo huna budi kukubaliana na mimi kwamba maendeleo ya sayansi na teknolojia yamekuja kuathiri sana watu kimtizamo pamoja na hata namna wanavyojiona! kwanini nasema maendeleo haya yamebadilisha watu kimtizamo?  Sababu kubwa inayonisukuma niseme hili ni kwa sababu watu wengi wamejikuta wakitumia sayansi na teknolojia kama kioo cha kujitizamia! Ambapo mwisho wa siku wanaishia kujiona wao ni wabaya kimuonekano, (hasa wakihusisha na rangi zao pamoja na muonekano wa maumbile yao) Kutokana na hilo wanaanza kujishushia thamani na kujiona wao kama siyo kitu, pasipo kujua kwamba kioo walichotumia kujitizamia siyo kioo halisi! Kwa mfano maendeleo ya sayansi na teknolojia yamekuja na ugunduzi wa baadhi ya viungo bandia (vinavyopandi...

Fahamu Jinsi Ya Kubadili Mitizamo Ili Ubadili Namna Unavyojiona...

Image
Kila mtu yupo hapa duniani kukua ili ayafikie mafanikio, na hakuna mtu ambaye yuko radhi ajione akibaki katika kiwango kilekile ilihali siku  zinazidi kwenda mbele! Na ifahamike kwamba, kadiri siku zinavyozidi kwenda mbele kila mtu anaukaribia utu uzima na hakuna ambaye anakua kuelekea utotoni! Kwa mantiki hiyo huna budi kukuza kiwango chako cha kujiona kipate kukua siku hadi siku. Mantiki yake ikiwa, kile kiwango ulichokuwa unajiona jana kiwe tofauti na kile kiwango utakachojiona leo! Na, itafaa zaidi endapo leo utajiona katika kiwango bora zaidi ya kile ulichojiona jana! Hata hivyo, itakuwa ni ajabu sana kuona mtu anabaki katika kiwango kilekile cha ufahamu wa kujiona ilihali umri wake unazidi kwenda na siku zinazidi kwenda mbele Hivyo basi ili ubadili namna unavyojiona huna budi kufanya yafuatayo: 1. Badili Fikra Zako Fikra zako zinaweza kukutoa hatua moja na kukupeleka hatua nyingine kwa sababu fikra ni vitu halisi ijapokuwa hazionekani. Umekuwa hivyo ulivyo, umefik...

Kwanini Watu Wengi Hujiona Vile Wajionavyo?... sehemu ya pili

Image
Makala iliyopita ilifanikiwa kudokeza sababu tatu ambazo humfanya mtu ajione vile ajionavyo. Sababu hizo zilikuwa ni kama zifuatazo: 👉Historia ya malezi 👉Mazingira 👉Marafiki Makala hii ni mwendelezo wa somo lililopita! Ninakukaribisha sana twende pamoja! Tuendelee na sababu ya nne: 4. Elimu Uliyopokea/Uliyopewa Kile unachokijua kupitia elimu uliyonayo ndicho kitakachopima umbali utakaoishia kujiona!  Kwa mantiki hiyo endapo utajua vitu vingi utajiona katika uweza, ukuu na ubora, ikiwa endapo utajua vitu vichache utajiona wewe ni duni, dhaifu na huwezi, hivyo utaishia kuwa na mitizamo duni dhidi yako!  Kwa namna moja ama nyingine elimu nayo, kama sababu ni moja ya kitu ambacho kimechangia kwa kiasi kikubwa katika kuwafanya watu wajione katika viwango duni. Suala hili limechangiwa sana na kile wanachofundishwa shuleni! Yaani kile kinachoingizwa ubongoni mwao kupitia elimu wanayoipata! Unachopaswa kujua ni kwamba, elimu nyingi za kitaaluma, hazina utaratibu wa kuwa...

Kwanini Watu Wengi hujiona vile wajionavyo?

Image
Kila kitu hutokea kutokana na sababu! Kwamba kuna kila sababu iliyopelekea kutokea kwa kila matokeo unayoyaona kwenye maisha yako! Unatakiwa kujua kwamba, hata hivyo unavyojiona ni kutokana na sababu ambazo zimekufanya ujione hivyo! Zifuatazo ni sababu ambazo zimekufanya ujione hivyo unavyojiona: 1. Historia Ya Malezi Sisi sote ni matokeo ya historia zetu, kwamba tumekuwa hivi tulivyo kutokana na kile historia imetufanya! Kutokana na ukweli huo huna budi kufahamu kwamba, historia ya malezi ndiyo imewafanya watu wengi wajione wao ni duni, dhaifu na hawawezi!  Na, ndiyo maana watu wengi tunajiona sisi ni wanyoge, hatuwezi, ni wadhaifu, hatustahili pamoja na kujiona kuwa hakuna kitu cha maana tunachoweza kukifanya hapa duniani! Kwa mfano kama ulipokuwa mtoto:  ulikosolewa sana, ulidharauliwa sana, uliitwa majina ya ajabu pamoja na kufananishwa na viumbe vya ajabu, ulipigwa sana, ulipokea manyanyaso ya hapa na pale, ulizuiwa kuongea, uliambiwa huwezi kufanya jambo Fula...

Huwezi Ukawa Mtu Ambaye Hujamuona...

Image
Awali kwenye makala iliyopita niliishia kudokeza kuhusu andiko lililopo kwenye methali 23:7 "maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo"  Sasa tuendelee... Unatakiwa kujua kwamba vile unavyojiona ndani ya nafsi yako, ndivyo unavyokuwa nje ya maisha yako! Na, ndiyo maana kisaikolojia inaaminika kwamba, kila kitu huanzia ndani ya nafsi kwanza, ndipo sasa hujidhihirisha nje. Hivyo basi, endapo ndani ya nafsi yako utajiona wewe ni fungu la kukosa, mnyonge na si kitu nawe utakuwa hivyo nje ya maisha yako.  Na ndiyo maana kanuni ya mwitikio na vitendo inasema kwamba; “matendo yako ni mwitikio wa fikra zako mwenyewe"  Hii inamaanisha kuwa, utaonesha mwitikio fulani kutegemeana na fikra ulizoziwasilisha juu ya namna ulivyojiona, na mwitikio huo unaweza kuwa wa kipumbavu au wa kikuu! Na, ifahamike kwamba upumbavu au ukuu wa mwitikio wako, utategemeana na aina za fikra utakazokuwa umeziwasilisha kukuhusu wewe mwenyewe!  Kutokana na hilo huna budi kufahamu kuwa mais...

Vile Unavyojiona Ndivyo Unavyokuwa…

Image
Hivi unafahamu kwamba zaidi ya asilimia 80 ya watu hujiona katika kiwango cha chini sana kiasi kwamba wanashindwa kuvuta hali nzuri maishani mwao? Unatakiwa kujua kwamba hakuna mwanadamu yeyote yule ambaye huenda mbali zaidi ya pale alipoishia kujiona. Hata hivyo huna budi ufahamu kwamba vile unavyojiona, ni sawa na unatengenezea ramani itakayokuongoza na kukufikisha pale ulipoishia kujiona. Hii inamaanisha kwamba pale ulipoishia kujiona ndipo palipo na ukomo wako.  Kwamba utakomea hapo na huwezi kwenda zaidi ya hapo katika kuishi kwako.  Na, ndiyo maana ni muhimu sana kuwa makini na mitizamo unayoitengeneza kuhusu wewe na maisha yako kwani hizo ni sawa na ramani zitakazokutoa sehemu moja na kukupeleka sehemu nyingine kimaisha.  Kwa mujibu wa tafiti binafsi nilizozifanya nimegundua kwamba watu wengi tunaongozwa na ramani zisizo na ukweli wowote ule, hali ambayo imetuponza wengi na kufanya maisha yetu yabaki duni na yasiendelee kabisa!  Kwa mfano tuchukuli...

Madhara Ya Kuamini Katika Imani Potofu... Sehemu ya Pili

Image
Makala iliyopita ilidokeza Madhara manne yasababishwayo na kuamini katika imani potofu! Kwa kukumbusha tuliona Madhara Yafuatayo: Utampoteza Mungu Katika Maisha Yako. Utaendelea Kubaki Na Hofu Hutojijua Wewe Ni Nani Utashindwa kubadili maisha yako! Kwa siku ya leo tutaona Madhara Mengine Kama ifuatavyo: 5. Utavuta matukio Hasi Maishani Mwako Ni kweli kabisa kwamba makwazo hayana budi kuja lakini ole wake  yule ayasababishaye. Sasa Kwanini ujisababishie makwazo kwa kuamini katika imani potofu? Unachopaswa kujua ni kwamba, matukio yote uliyokutana nayo pamoja na hali zote unazopitia katika maisha yako ni mambo yanayotokana na mfumo wako wa kuamini!  Yamkini umaskini umekuzonga, huenda mahusiano yako ni tete, yamkini hali yako ya kiuchumi ikawa ni ngumu sana, yamkini biashara yako haifanyi vizuri, yamkini marafiki zako wamekutenga, yamkini upo gizani na umekata kabisa tamaa, yamkini unapitia maumivu makali sana wakati huu na huenda umepoteza kabisa mpaka hamu ya kuish...

Madhara Ya Kuamini Katika Imani Potofu...

Image
Makala nilizofanikiwa kuzituma hapo awali zilidokeza kuhusu jinsi imani huwa haimsaliti muamini wake! Kutokana na hilo msisitizo mkubwa ukawekwa kwa kumtaka kila muamini aamini kwenye imani thabiti!  Kwa leo naenda kudokeza Madhara Ya Kuamini Katika Imani Potofu!  Madhara hayo ni kama ifuatavyo:   1. Utampoteza Mungu Katika Maisha Yako… Mungu hapendi watu wenye imani ya kusitasita kwa maana hao hawawezi kujibiwa maombi yao. Watu hawa hawana imani juu ya uweza wa Mungu, hii inamaanisha kwamba, hata wanapoomba wanatilia shaka kile waombacho kuwa hakitawezekana, na kweli hakitawezekana kwa sababu imani yao ipo kwenye kutokuwezekana... Kutokana na hilo watajikuta wakishindwa kutambua uweza na nguvu za Mungu katika maisha yao, hali itakayowapelekea washindwe kumpa Mungu nafasi kwenye maisha yao! Kwa kulitambua hilo ndiyo maana Yakobo 1:6 inasema; " Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo...

Tatizo Siyo Kilichotokea Tatizo Ni Kile Unachokiamini...

Image
Mpenzi, unatakiwa kujua kwamba imani potofu ndiyo hupelekea upate matokeo hasi, kwa maana imani yako haiwezi kukusaliti wewe muamini wake! Hivyo basi endapo utaamini katika dhana potofu matokeo yake yatakuwa ni kupotea... Kwani nawe utapokea kwa kadri ya uaminivyo! Na ifahamike kwamba, ni kupitia kuamini katika imani potofu ndiko kumekuwa kukiangusha jitahada zako pamoja na juhudi zako, kwani hata ukifanya juhudi huoni kama zitakulea matunda kwa kuwa umeamini kwamba wewe huwezi na si chochote kile... Hii inamaanisha kwamba ni vigumu sana kupata hamasa ya kufanya jambo fulani, kwa sababu hata ukifanya imani yako inakuona wewe ni fungu la kukosa, na hakuna kitu cha maana unachoweza kukifanya au kukipata...  Hata hivyo kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kisaikolojia kuwahi kufanyika, zimeonesha kwamba mwanadamu huteseka zaidi kifikra kuliko uhalisia. Unatakiwa kujua kwamba, unapofikiri kuwa jambo Fulani lipo hivi, maana yake unaanza kutengeneza imani kuhusu jambo hilo kwen...

Tatizo Siyo Kilichotokea Tatizo Ni Kile Unachokiamini... ni

Image
Hivi unafahamu kwamba zaidi ya asillimia 80 ya watu wanaamini zaidi katika imani potofu, kuliko imani thabiti hali ambayo hupelekea anguko lao?  Unatakiwa kujua kwamba imani ni kama mbegu, ambayo ikipandwa humea, ikishamea hukomaaa, ikishakomaa huzaa matunda ya aina yake, ikishazaa matunda basi matunda hayo huchumwa… Mlolongo huo unaonesha ni kwa namna gani unapoamini katika jambo Fulani ndivyo unavyokuja kulivuna jambo hilo kutegemeana na ile imani uliyoipanda kuhusu jambo hilo… Mpenzi msomaji unatakiwa kujua kwamba kuamini ni kupokea kuwa jambo Fulani ni kweli hata kama jambo hilo halipo hivyo… Kutokana na hilo ni dhana potofu kuamini katika imani potofu kwani kile utakachokiamini kuwa kipo vile kitakuja kutokea kama vile wewe mwenyewe ulivyokiamini... Na, ndiyo maana hata kanuni ya kuamini inasema, “chochote utakachokiamini kuhusu wewe na dunia yako kitafanyika kwako kama uaminivyo” Unatakiwa kujua kwamba kanuni hii inafanya kazi kwenye imani thabiti au imani potofu....

Jinsi Ya Kupata Matokeo Unayoyataka. Mbinu Ya 6,&7

Image
6. Jua Gharama Zitakazohitajika Pamoja Na Kuwa Tayari Kulipa Gharama Kwa kila matokeo mazuri na ya maana utakayoyataka ni lazima kuna gharama utatakiwa kulipa kwanza! Rafiki, huwezi kupata matokeo unayoyataka pasipo kujua gharama zitakazohitajika ili uweze kupata matokeo hayo! Hii ni sawa na kusema, ili uweze kupata matokeo yoyote yale yaliyo mazuri ni lazima kuna gharama unatakiwa uwe tayari kuzilipa. Na ifahamike kwamba, kujua matokeo unayoyataka siyo kigezo cha wewe kuyapata bali ni lazima ukubali kulipa gharama zitakazohitajika ili upate matokeo hayo! Hivyo basi unachopaswa kufanya hapa ni kuchagua matokeo unayoyataka, baada ya hapo jua gharama zitakazohitajika, na ukishazijua gharama hizo kuwa tayari kuzilipa ili uweze kupata matokeo unayoyataka.  Kumbuka tupo kwenye ule ulimwengu ambao kitu unachoweza kukipata bure ni salamu tu, cha ajabu ni kwamba watu wenye siku hizi hawasalimii sijui uungwana unapotelea wapii? Hata hivyo unatakiwa kujua kwamba gharama zitakuwa ...

Jinsi Ya Kupata Matokeo Unayoyataka, mbinu ya 4&5

Image
4. Jiweke Huru Kutoka Kwenye Vikwazo... Kwa chochote kile utakachoazimia kukifanya lazima kuna vikwazo huibuka! Kwa mantiki hiyo usipojiweka huru kutoka kwenye vikwazo hivyo hutapata matokeo unayoyataka!  Rafiki, unatakiwa uvikabili vikwazo vyote ambavyo vitakufanya ushindwe kupata matokeo yale unayoyataka!  Hata hivyo kuna baadhi ya vikwazo vingine huwa vipo nafsini mwako kwa hiyo huna budi kuanza nafsi yako kwanza! Kwa maana moja ya sababu ambazo hutatiza ndoto za wengi ni ile hali ya mtu kujiona hawezi na hastahili! (Self limiting beliefs) Rafiki hutakiwi kujiona, huwezi, hustahili, wewe ni duni, wewe ni dhaifu na unatokea kwenye familia ya kimaskini.  Endapo utajiona hivyo,  ni dhahiri kabisa hutaweza kupata matokeo yale unayoyataka!  Kwa maana hutopata hamasa na motisha ya kufanya juhudi ili upate kile unachokitaka! Mbali na hilo Kanuni Ya Vikwazo inasema; “kwa chochote kile utakachoazimia kukifanya lazima kuna vikwazo vitaibuka”. Hata hivyo mba...