Posts

Showing posts from May, 2024

Jinsi Ambavyo Walimu Wa uongo Hupelekea Watu Wajifunze Yasiyofaa...

Image
Kitaaluma mimi ni mwalimu mtaalamu. Nikiwa kazini kuna wakati wanafunzi huwa wananiita mwalimu! Mwalimu! Nami huwa naitika kwa kusema; “mwalimu wa pekee na wa kweli alikuwa Yesu Kristo”  Simaanishi kwamba walimu wengine hawafai lahasha! Tafadhali usinielewe vibaya, walimu wazuri wapo. Hata hivyo uzuri wa mwalimu unapimwa kupitia maarifa anayoyatoa kama yanajenga au yanabomoa.  Endapo itatokea mwalimu akawa anatoa mafundisho yanayoharibu, kudidimiza na kubomoa badala ya kujenga basi mwalimu huyo hafai, bali anachokifanya ni uharibifu.  Mwalimu huyu anastahili kupewa jina la mwalimu mharibifu na si jina la mwalimu mjenzi kwa sababu anachokifanya ni kuharibu akili za watu!  Hawa ndiyo walimu tulionao karne hii, kwa sababu ukichunguza kwa ukaribu utagundua kwamba karibu kila sekta tumezungukwa na walimu, lakini ujinga bado ni mwingi kumbe tatizo siyo ujinga, bali tatizo ni walimu wenyewe kutokana na mafundisho wanayoyatoa!   Mtu anapobaki kuwa mjing...

Jinsi ambavyo Umaskini Huwafanya Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...

Image
Katika safari ya kuishi kwangu na kujifunza nimekuja kugundua kuwa, maskini huwa hana chaguo! Ukweli ni kwamba maskini ni sawa kabisa na yatima ambaye huwa hadeki!  Kwa kusema hivyo hapa duniani kuna elimu maalumu kwa ajili ya matajiri na kuna elimu maalumu kwa ajili ya watu maskini. Hii ni sawa na kusema Tajiri atapokea elimu nzuri kwa sababu ana uwezo wa kuimudu kwa kulipa gharama, kwa maana hakuna kitu kizuri ambacho hupatikana bure au hupatikana kwa bei rahisi.  Na elimu hiyo ambayo matajiri hupokea huwa inalenga kufundisha mambo halisi yaliyopo kwenye mazingira waliyopo ili watumie taarifa hizo katika kutengeneza utajiri!  Kwa mfano elimu hiyo hufundisha masuala ya uwekezaji pamoja na ugunduzi na uvumbuzi. Kwa mantiki hiyo ni ngumu sana kuona Tajiri akipitishwa kwenye mitaala ya zamani ambayo haimpi taarifa sahihi zinazoihusu dunia tuliyonayo sasa!  Nakusanua tu nenda kapitie kwenye mitaala ya nchi zilizoendelea ndiyo utagundua uhalisia wa kile ninac...

Fahamu jinsi Kasumba Ya Kutaka Kukubalika Huwafanya Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...

Image
Kisaikolojia inaaminika kwamba karibu kila jambo ambalo mwanadamu hulifanya maishani mwake, huwa limelenga Zaidi kumfanya akubalike na watu wengine.  Na hii ndiyo sababu ambayo huwafanya watu wengi wasome shule nzuri, hata kama elimu wanayopokea haiwasaidii katika kuwafungua kiufahamu na kifikra, wahitimu kutoka vyuo vikuu maarufu na vizuri duniani, n.k Unatakiwa kujua kwamba haya yote hufanyika ili kumfanya huyo mtu akubalike na wengine kutokana na hadhi yake, ikiwa ni pamoja na kumfanya aonekane yu mtu mkuu mbele ya wenzake. Na ndiyo maana watu waliosoma hujisifu sana na hujiona kama wanajua vitu vyote, kumbe wanavyovijua ni vichache tena visivyowasaidia na wasivyovijua ni vingi tena vilivyo na msaada mkubwa sana maishani mwao! Ngoja nikuulize swali la kizushi, hivi lengo lako la Kwenda shule kwa ajili ya kusoma lilikuwa ni nini, je, kukombewa kifkira ama Kukubalika? Unaweza ukawa hujui vilevile, kwa sababu wengi walienda shule kutokana na msukumo uliotoka kwa wazazi ...

Jinsi Ambavyo Mazingira Hupelekea Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...

Image
Vitu vingi ambavyo mwanadamu anavifanya vinatokana na msukumo wa  mazingira yanayomzunguka mwanadamu huyo!  Kwa kusema hivyo mtu huyo atajikuta akifanya baadhi ya tabia si kwa sababu anatakiwa afanye tabia hizo bali atajifunza kufanya tabia hizo kama moja ya mbinu ya kuyakabili na kuingiliana na mazingira yanayomzunguka! Sasa hapa itategemeana na aina mazingira yanatakayokuwa yanamzunguka mtu huyo aidha ni mazingira mazuri au mazingira mabaya! Na ifahamike kwamba, mazingira ni nguvu isiyoonekana ambayo humtawala mwanadamu kifikra, kimaono, kimatendo, kimtizamo na kimienendo.  Ukweli ni kwamba kila mtu ni tunda linalotokana na mazingira anayotokea. Hii ni sawa na kusema kuwa, hivyo ulivyo ni kutokana na kile ulichojifunza kutoka kwenye mazingira unayotokea. Unatakiwa kujua kwamba kuna watu wamekuwa na fikra za uhaba/mgando kwa sababu ni kitu ambacho wamejifunza kutoka kwenye mazingira walimokulia, lakini haimaanishi kwamba walitakiwa wawe hivyo!  Ukiachili...

Kama Huna Malengo Sahau Kabisa Kujifunza Vitu Sahihi Maishani Mwako...

Image
Hivi unafahamu kwamba asilimia kubwa ya watu wengi hapa duniani huishi pasipo malengo maishani mwao hali ambayo huwafanya washindwe kutofautisha mafunzo sahihi na mafunzo yasiyo sahihi? Ukweli ni kwamba kujifunza ni jambo ambalo huenda sawa na lengo la kujifunza, kwa hiyo inapotokea mtu akawa anajifunza lakini hana lengo lolote lile katika kujifunza kwake, maana yake mtu huyo ataishia kujifunza vitu visivyo na msaada maishani mwake! Hata mimi hapo awali kabla sijajitafuta nilikuwa ni mtu ambaye sikujua maana halisi ya lengo, na sikuwahi kuazimia lengo lolote lile maishani mwangu, kwa maana sikuwa na uelewa wowote ule kuhusu lengo! Kwa kusema hivyo nilikuwa naishi tu kwa vile niko hai, ila kule nilikokuwa naongoza maisha yangu nilikuwa sikujui, kutokana na hilo nikajikuta nikijifunza karibu kila jambo si kwa sababu ninatakiwa kujifunza ila ni kwa sababu sikuwa nimelenga chochote kile kwenye ujifunzaji wa mambo hayo! Matokeo yake sasa nilijikuta nikisoma hata vitu ambavyo sik...

Jinsi Ambavyo Marafiki Hupelekea Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...

Image
Mtu mmoja mwenye busara aliwahi kusema kuwa; “vile utakuwa miaka mitano ijayao itategemeana na marafiki ulionao pamoja na vitabu unavyosoma”.  Sote tumeona kwenye hiyo nukuu kuna neno marafiki. Huenda ukawa unajiuliza kwanini marafiki? Unatakiwa kujua kwamba akili yako inajua jinsi ya kuendana na wengine, kwa mantiki hiyo unapochangamana na marafiki fulani Fulani hivi maana yake akili yako itakusukuma na wewe uenende kama wao wanavyoendana, kwa sababu ni vitu ukavyojifunza kutoka kwao. Unaweza ukawa unajiuliza kwanini akili yangu hujifunza kutoka kwa marafiki zangu?  Jibu ni jepesi tu, jambo hili la kujifunza hufanyika ili kukuwezesha ukubalike kwenye kundi la marafiki unalohusiana nalo.  Kwa kusema hivyo, endapo marafiki zako watakuwa ni watu wenye mitizamo hasi, ni watu wenye mienendo mibovu, ni watu wasiojali kesho zao hata wewe utajifunza na kuwa kama wao walivyo! Ukweli ni kwamba kuna baadhi ya watu ambao kabla hawajawa na aina fulani hivi za marafiki, wa...

Jinsi Ambavyo Jamii Hupelekea Watu Wajifunze Vitu Visivyo Sahihi...

Image
Neno jamii linamaanisha muunganiko wa koo mbalimbali zilizo tofauti zinazokaa katika eneo Fulani la kijiografia, zinazochangia sifa Fulani Fulani hivi fananifu kama vile: lugha, historia moja, uongozi mmoja pamoja na mila na desturi. Na, kwa vile jamii huchangia sifa Fulani hivi fananifu, hii inamaanisha kwamba hata Imani yake na mitizamo yake huwa inafanana kwa jamii yote! Na, ndiyo maana ni rahisi sana kuweza kuigundua jamii ya watanzania kwa kuangalia mtindo wao wa kuishi ulivyo. Na kwa vile jamii hujumuisha watu wengi, maana yake ndani yake kuna mengi ya uozo yanayofanyika.  Na, ifahamike kwamba suala la kujifunza lipo automatiki, kwa kusema hivyo kupitia jamii tuliyonayo kuna watu wamejifunza vitu visivyo sahihi kama vile vinavyofanywa na baadhi ya wanajamii! Ukweli ni kwamba chini ya mwamvuli wa jamii kuna watu wamejifunza kuwa, kwa vile wamezaliwa kwenye jamii maskini hawawezi kufanikiwa kifedha na kimaisha kiujumla.  Kadhalika chini ya mwamvuli wa jamii kun...