Posts

Showing posts from July, 2023

Je Umekuwa Ukikumbwa Na Hofu Maishani Mwako? Hizi hapa Ni Sababu Ambazo Hupelekea Hofu...

Image
Kwa mujibu wa kanuni ya kichocheo na matokeo inadai kwamba, "kila kitu hutokea kutokana na sababu" Hii inamaanisha kwamba, kama hakuna sababu basi hakuna matokeo. Na, hii ni kwa sababu kila matokeo / hali hutokana na kisababishi fulani. .. Hii ni sawa na kusema hauhofii tu kwa sababu  unatakiwa uhofu, ila unahofia kwa sababu kuna visababishi vilivyopelekea uweze kuhofu... Ukweli ni kwamba hofu ni kama ugonjwa ambao humfanya mtu awe mahututi, na endapo mtu huyo hatazinduka anaweza akafa katika hali ya unyonge na asifurahie kabisa maisha yake hapa duniani. Zifuatazo ni sababu ambazo hufanya watu wengi wawe na hofu maishani mwao... 5. Kukisa maarifa/Taarifa Sahihi… Hosea 6:4 “…kwa kuwa umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe…" Kama unakuwa kimwili kutokana na kile unachokula, vilevile utakuwa kiakili kutokana na kile unachoulisha ubongo wako.  Kukosekana kwa mwamko wa kujifunza kumefanya watu wengi wazidi kuwa na hofu kwa sababu ya kukosa, maarifa pamoja ...

Fahamu Kuhusu Mgawanyiko Wa Hofu Za Kujifunza...

Ni Lini Utaacha Kuutumikia Utumwa Wa Hofu Usiokuwa Na Manufaa?...

Image
Hivi unafahamu kwamba zaidi ya 80% ya watu duniani kote wanaishi maisha yaliyojaa hofu, wasiwasi pamoja na mashaka kiasi kwamba wanakosa kabisa hata uthubutu wa kutoka pale walipo na kwenda hatua nyingine ya juu zaidi?  Huenda hata wewe ukawa ni miongoni mwa watu hao ambao pasipo kujua wamejikuta wakiipa hofu mamlaka ya kuendesha na kutawala maisha yao, kuliko hata wao wenyewe walivyojipa mamlaka na ukuu wa kutawala na kuongoza maisha yao. Ukweli ni kwamba hakuna uhalisia wa kitu ambacho huwa kinaogopwa, bali nafsi ya mtu kupitia fikra zake ndizo humuweka mashakani.  Na, ifahamike kwamba kila kitu katika maisha ya mwanadamu huanzia ndani ya nafsi yake kwanza ndipo sasa hujidhihirisha nje ya maisha yake.  Hii inamaanisha kwamba hata hofu hutengenezwa… Na, uhalisia wa jambo hili unajidhihirisha kwenye kanuni ya uakisi wa mambo ambayo inasema: “ulimwengu wako wa nje ni uakisi wa ulimwengu wako wa ndani” hii inaamanisha kwamba vile unavyotengeneza hofu ndani ya na...

Sahau Kabisa Kubahatika Mpaka Usome Kwanza Hii...

Image
Makala iliyopita ilidokeza hoja nne kuhusu namna gani unaweza ukaivuta Bahati Maishani Mwako! Leo umeletewa mwendelezo wa somo hili, ungana na wanafamilia wenzako ambao wamekuwa wakifuatilia masomo haya pamoja na kunufaika nayo! Je unataka uvute bahati ije katika maisha yako?... Kama jibu lako ni ndiyo basi kuna ujumbe wako mzuri hapaa... 5. Fanya Jambo Litakalopelekea Bahati Yako Kwa Mwendelezo... Hutakiwi kuwa mtu wa kufanya mambo kwa kudonoa donoa wala kwa ulegevu, bali unatakiwa kila siku ufanye jambo Fulani litakalokusogeza pale ambapo hatima ya bahati yako ilipo!  Kuna kanuni moja inaitwa kanuni ya mlimbikizano, kanuni hii inasema kwamba “unapata matokeo makubwa kutokana na kufanya mambo madogo kwa mwendelezo ndani ya kipindi cha muda fulani” Sikiliza my friend, sharti la kupata matokeo makubwa (bahati yako) liko wazi kabisa kwamba, ni lazima ukubali kufanya mambo madogomadogo kwa mwendelezo ndani ya kipindi cha muda Fulani.  Na endapo hutafanya kwa mwendelez...

Nifanye Nini Ili Nivute Bahati Maishani Mwangu?

Image
Mithali 22:29 “Je, wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake? Huyo atasimama mbele ya wafalme, hatasimama mbele ya wasio na cheo” Neno liko wazi kabisa kwamba bidii ndiyo mbegu  sahihi ya bahati ni siyo kukaa tu huku ukingojea upepo!  Kwa mantiki hiyo ukiona mtu amesimama mbele ya wafalme, watu wakuu na wenye vyeo pamoja na kufanya mambo makubwa haimaanishi kwamba ana bahati bali bidii yake ndiyo imemstahilisha! Najua unajiuliza ninaweza nikafanya nini ili niweze kuvuta bahati maishani mwangu? ...Usijali ndani ya muda mfupi ujao unaenda kugundua siri kubwa sana zinazoenda kubadilisha kabisa maisha yako... Je unataka kuvuta bahati maisha yako? Kama jibu ni ndiyo huna budi kufanya yafuatayo: 1. Pata Maana Kamili Ya Bahati... Katika hali ya kawaida huwezi ukavuta kitu katika maisha yako ambacho hata wewe mwenyewe hukijui vizuri.  Kwako wewe bahati ni nini? Je, ni kuokota nyumba? Je, ni kuokota gari? Je, ni kuokota kiasi kingi cha fedha? Je, ni kupata kazi nzuri? ...

Ukweli Unaopaswa Kuujua Kuhusu Bahati. sehemu ya pili

Image
makala iliyopita ilidokeza hoja tatu kuhusu asili ya bahati. Kama ulivyoahidiwa toka juzi kwamba kutakuwa na mwendelezo wake basi leo utafahamishwa hoja nyingine zaidi kuhusu asili ya bahati! Fuatana nami, ukajionee mwenyewe! 4. Bahati Huwakuta Wale Wanaoiamini Kuwa Ipo. Huwezi ukakivuta kitu ambacho hujakiamini kwamba kipo kwa ajili yako!  Sasa utaivutaje bahati katika maisha yako ilihali umeamini kwamba wewe una mikosi, una laana na huna bahati? Mpenzi unatakiwa kujua kwamba kile unachokiamini ndicho unachokivuta katika maisha yako!  Hivyo basi endapo utakuwa unafanya juhudi zako, huku ukiamini kwamba katika juhudi zako kuna siku utabahatika, ama hakika utavuta bahati katika maisha yako kutokana na imani ilile uliyoiweka kwenye juhudi zako! Unatakiwa kujua kwamba kuamini ni kupokea kuwa jambo Fulani ni kweli hata kama jambo hilo siyo kweli. Lakini msisitizo upo kwenye kufanya juhudi, kwamba utakuwa ni upumbavu kuamini kuwa siku yako ya bahati inakuja ilihali haku...

Ukweli Unaotakiwa Kuujua Kuhusu Bahati…

Image
         Mhubiri 9:11 “nikarudi nikaona chini ya jua, ya kwamba siyo wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala si wenye ustadi wapatao upendeleo lakini wakati na bahati huwakuta wote” Kifungu cha ufunguzi kimedokeza kwa lugha ya uwazi kabisa kwamba bahati na wakati huwakuta wote haijalishi wewe ni nani! Kwa minajiri hiyo ni sawa na kusema kwamba, ukifanya jambo sahihi kwa namna sahihi na kwa wakati sahihi huku wewe mwenyewe ukiwa ni mtu sahihi kuna uwezekano mkubwa sana wa wewe kuvuta bahati katika jambo hilo…  Ngoja nikudokezee ukweli unaopaswa kuujua kuhusu bahati! 1. Kila Mtu Ana Bahati… Mpenzi msomaji una bahati kubwa sana kuzaliwa ukiwa hai na mpaka sasa unaishi! Kwani siyo kila kinachozaliwa kinaishi! Unatakiwa kujua kwamba kuzaliwa ni kitu kingine na kuishi ni kitu kingine! Tumshukuru Mungu kwa bahati ya uhai aliyotujalia! Un...

Je, Mshindi Wa Bahati Nasibu Akitangazwa Mshindi Ile Nayo Ni Bahati?

Image
Makala iliyopita awali ilidokeza baadhi ya mitizamo ya watu wengi kuhusu Bahati.  Hitimisho lake lilionesha kwamba watu wengi huishia kuona bahati kama tukio, na siyo kuona bahati kama mchakato wa kupelekea tukio la kufurahisha! Unachotakiwa kujua ni kwamba, kiuhalisia bahati kama bahati haipo bali mchakato wa kutengeneza bahati ije itokee ndiyo upo na huo mchakato ndiyo bahati yenyewe sasa!  Kwa leo naenda kujibu swali litakalokupa uelewa kuhusu maana halisi ya bahati.  Je Mshindi Wa Bahati Nasibu Akitangazwa kuwa Mshindi huwa anakuwa amepata bahati? ...Imenibidi nitumie mfano usio rasmi ili kukuelewesha zaidi kuhusu maana ya halisi ya bahati! N.B usiende kufanya kile ninachoenda kukidokeza kwenye mfano huu…  Bali tumia kama muongozo kwenye eneo unalotaka bahati ikukute!  Bila shaka umeshasikia kuhusu washindi wa bahati nasibu, na huenda hata wewe mwenyewe mwenyewe umejaribu mara kadhaa kushiriki kwenye michezo hiyo! Sijui kama ushawahi kushinda au ...

Onyo Hata Usifikirie Kubahatika Mpaka Usome Kwanza Hii...

Image
Hivi unafahamu kuwa zaidi ya asilimia 80 ya watu wanasubiri bahati iwafike ndipo waweze kubadili maisha yao, pasipo kujua kuwa wanachosubiri ni upepo (usio kitu) na siyo bahati kama wao wanavyodhani? Bahati ni neno dogo sana ambalo limewanasa watu wengi sana kwenye mtego, na wengi bado wanaendelea kunaswa kwenye mtego huo. Na, hii ni kwa sababu katika maisha yao hakuna chochote kile cha maana wanachokifanya, zaidi ya kusubiri mungubahati awatembelee nao wapate kubadilisha maisha yao....  Hebu jaribu kufanya uchunguzi wa chinichini utagundua kuna kundi kubwa la watu ambalo limekaa tu, huku likiwa halijishughulishi na chochote kile. Hata hivyo mbali na kutokujishughulisha, bado linaamini kwamba kuna siku ya bahati inakuja bado, ambayo itakuja kubadili mazima historia ya maisha yao... Hali hiyo imewafanya watu wengi wajihesabie haki  na kuona kubahatika ni haki yao, na hata wasipojishughulisha ni sawa tu kwa maana siku ya bahati yao haijaja bado! Ukweli ni kwamba watu...

Njia Kuu Tatu Rahisi Za Kubadili Mitizamo Yako Juu Ya Namna Unavyojiona...

Image
4. Jione Sawa Na Vile Muumba Wako Akuonavyo... Vile Muumba anavyokuona huenda ikawa ni tofauti kabisa na wewe unavyojiona!  Kwamba wewe unajiona kwa namna hii ikiwa Mungu anakuona kwa namna nyingine!  Kwa mfano unaweza ukajikuta unajiona huwezi, hustahili na si kitu, lakini Mungu akawa anakuona kuwa unaweza, unastahili na wewe ni mtu wa thamani sana kuwahi kutokea hapa duniani! Na ifahamike kwamba, Mungu wetu ni Mungu wa yawezekanayo na si Mungu wa wasiyowezekana, hivyo basi endapo utajiona kama yeye akuonavyo kwako wewe kila jambo litawezekana. Hebu tuangalie maandiko matakatifu yanachosema kuhusu vile Mungu atuonavyo: "Ee bwana umenichunguza na kunijua, Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;   Umelifahamu wazo langu tokea mbali". Zaburi 139 "Kabla sijakuumba katika tumbo la mama yako nalikujua na kabla hujatoka tumboni nalikutakasa"… “Yer 1:5”.  Friend, umeona Sasa? Mungu anakujua wewe vizuri kuliko hata wewe mwenyewe unavyojijua! Unatakiwa k...