Posts

Showing posts from January, 2024

Je Ungependa Kuyajua Maeneo Kumi Ambayo Fedha Imejificha...?

Image
Habari yako rafiki yangu! Ni matumaini yangu u mzima wa afya! Karibu kwenye mwendelezo wa somo letu linaloangazia kuhusu maeneo kumi ambayo fedha Imejificha! Kama unakumbuka vizuri makala iliyopita ilidokeza maeneo matatu, makala hii ni mwendelezo wa makala iliyopita! Sasa unaweza kusonga nayo kwa kuyapitia  maeneo mengine matatu kati ya kumi ambayo fedha imejificha kama ifuatavyo:- 4. Fedha imejificha kwenye fursa Tatizo la mtu moja ni fursa ya mtu mwingine kutengeneza fedha, na ndiyo maana ikitokea mtu amekuja kwangu kuuliza jambo kuhusu tatizo fulani, huwa nalichukulia tatizo lake kama fursa ya kutengeneza fedha.  Kutokana na hilo huwa nasimama kama mtu wa kutatua tatizo lake, na kama itashindikana huwa nasimama kama dalali wa kumuunganisha na mtu mwingine atakayemtatulia tatizo lake kwa kamisheni! Kumbuka awali tuliona kwamba matatizo ya watu ni fursa za kutengeneza fedha!  Hata hivyo wapo watu ambao hudhani kufanikiwa kifedha ni bahati, kitu ambacho siyo ...

Kama Unataka Kuvuta Fedha Maishani Mwako Nitakuonesha Maeneo 10 Ambayo Fedha Imejificha ....

Image
Ukimuuliza mvuvi ni namna gani ya kunasa Samaki kirahisi atakuambia maeneo yote ya Bahari ambayo Samaki hujificha!  Na katika kufanya shughuli zake za uvuvi basi huhakikisha, anatega nyavu zake maeneo hayo ili aweze kuwanasa samaki wengi kirahisi. Vivyo hivyo ndivyo ilivyo hata kwenye kuvuta fedha! Unatakiwa kujua kwamba kuna maeneo ambayo fedha imejificha, kwa kusema hivyo linapokuja suala la kutengeneza na kuvuta fedha maeneo hayo ni lazima yazingatiwe! Unatakiwa kujua kwamba endapo utakuwa unatafuta fedha pasipo uelewa wowote wa maeneo haya kumi ambayo fedha imejificha, hutokuwa tofauti na mtu anayetafuta bikira ndani ya wodi wazazi!  Yafuatayo ni maeneo kumi ambayo fedha imejificha, kwa mantiki hiyo katika safari yako ya kutafuta fedha hakikisha unaitafuta katika eneo mojawapo ya haya maeneo kumi! 1. Fedha Imejificha Kwa Watu... Dunia ya sasa ina watu Zaidi ya bilioni saba, na kila mtu unayemuona ana fedha mfukoni mwake.  Lakini mtu huyo hawezi kutoa fedha...

Umekuwa Hivyo Ulivyo Kutokana Na Aina Ya Marafiki Ulioamua Kuwa Nao...

Image
Kwa mujibu wa tafiti za kisaikolojia kuwahi kufanyika zimeonesha kwamba, akili ya binadamu inajua jinsi ya kuendana na wengine.  Kutokana na dai hilo unatakiwa ukubali ukweli huo ya kwamba, hata akili yako inajua jinsi ya kuendana na watu wengine.  Hii ni sawa kusema kuwa, huwezi ukafanya kitu kitakachokuwa tofauti na kile ambacho marafiki zako wanakifanya! Na, hii ni kwa sababu hautafanya mambo kwa sababu unatakiwa kufanya bali utajikuta ukifanya baadhi ya mambo kwa sababu watu wako wa karibu wanayafanya! Nioneshe watu wako wa karibu nami nitakwambia wewe ni nani. Msemo huu unamaanisha kuwa, watu unaoshinda nao muda wote ni utambulisho tosha kabisa kuhusu wewe ni nani hasa. Jambo moja unalotakiwa kuondoka nalo hapa ni kwamba, utajikuta ukitengenezwa automatiki kwa kuitikia na kufanya kile ambacho watu wako wa karibu wanakifanya. Na, itakuwa ngumu sana kwako kutokufanya kile ambacho watu wako wa karibu wanakifanya.  Hata hivyo, madai yenye mashiko ya kisaikolo...

Fahamu Jinsi Ambavyo Mfumo Wa Malezi Humtengeneza Mwanadamu Kifikra...

Image
Awali ya yote unatakiwa kujua kwamba, eneo la malezi ni eneo nyeti sana, ambalo ndilo kwa mara ya kwanza huhusika katika kumtengeneza au kumharibu mtu kifikra, kupitia taarifa zinazoingizwa ubongoni mwake! Na, ifahamike kwamba hakuna mwanadamu ambaye huzaliwa akiwa na ufahamu au uelewa wowote ule, suala hili lilithibittishwa na David Hume kupitia nadharia yake aliyoipa jina la blank slate/taburalasa! Hata hivyo kisaikolojia inaaminika kwamba, kile kitu ambacho mtoto hukutana nacho wakati wa ukuaji wake, ndicho humfanya awe vile alivyo! This is what we call the effect of conditioning... Ukweli ni kwamba wazazi au walezi ndiyo watu wa kwanza, ambao huingiza taarifa kwenye ubongo wa mtoto!  Na, taarifa hizo huweza kuwa mbaya au nzuri! Kinachosikitisha zaidi ni kwamba wazazi/walezi wengi huingiza taarifa hasi zaidi kwenye ubongo wa mtoto, na hii ni kwa sababu ya watu wengi kuwa na mitizamo hasi kuhusu maisha!  Hebu jaribu kurudisha kumbukumbu zako nyuma ulivyokuwa mtot...

Fahamu Jinsi Mfumo Wa Elimu Unavyoweza Kumtengeneza Mwanadamu Kifikra...

Image
Kanuni ya kinachoingia na kinachotoka inasema " kinachotoka huakisi kilichoingia" Kwa mantiki hiyo kama kilichoingizwa kwenye ubongo ni cha kijinga, kitakachotoka kitakuwa ni cha kijinga vilevile!  Hii ni kwa sababu ubongo wa mwanadamu hufanya kazi ya kuchakata matokeo na kufanya mambo yatokee, kwa kutumia taarifa zilizoingizwa na kuhifadhiwa ndani yake!  Hata hivyo, enzi za nyuma sana, dunia haikuwa na maendeleo yoyote ya kisayansi na kiteknolojia kama ilivyo sasa, kutokana na hilo watu waliishi kwa kufanya shughuli za kawaida kwa kutegemea mfumo walioukuta. Hata hivyo mara baada ya ugunduzi wa mashine zilizopelekea kuanzishwa kwa viwanda pamoja na maendeleo ya sayansi na teknolojia ukahitajika ujuzi wa aina mbalimbali. Kutokana na hilo elimu ikaanzishwa kwa lengo la kuwaandaa na kupata wafanyakazi ambao wangeweza kuendesha mashine mbalimbali viwandani. Hata hivyo,  mara baada ya wasomi hao tu kuhitimu walipata nafasi za kuajiriwa pamoja na kupewa mishahara ...

Fahamu Kuhusu Mifumo Ambayo Humtengeneza Mwanadamu...

Image
Kwa tafsiri nyepesi mifumo inaweza kufafanuliwa kama, ni taratibu/njia/miongozo ambayo hutawala, huongoza au husimamia utendekaji wa jambo Fulani kuanzia mwanzo wake hadi mwisho wake. (Yaani matokeo yake). Hii ni sawa na kusema mifumo hutawala jambo Fulani kutoka kuanza kwake hadi kukamilika kwake.  Kwa mfano tokea umezaliwa kuna mifumo Fulani ambayo uliingizwa nayo, ambayo imekuwa ikikuongoza, ikikutawala na kukusimamia hadi imekufanya umekuwa hivyo ulivyo.  Na, unaiona dunia kwa namna hiyo, kwa sababu kichwani mwako kuna taarifa zimeingizwa zinazokufanya uitafsiri dunia pamoja na vitu vilivyomo kwa namna hiyo.  Hata hivyo, katika ulimwengu wa saikolojia kuna kitu kinaitwa archetypes, hii ni mifumo Fulani ambayo ambayo humfanya mtu awe vile alivyo. Mifumo hii huwa ni jumla ya tabia zote ulizonazo yaani utambulisho wako!  Hii inamaanisha kwamba, mara baada ya kulelewa nayo kwa muda mrefu umejikuta ukianza hadi kutambulishwa kupitia mifumo hiyo. Na huenda ...

JINSI YA KUPANGA MALENGO KWA KUTUMIA NENO SMART..._____________________________

Neno smart ni kifupisho cha maneno matano, ambayo yanatoa sifa nzuri za lengo lililoazimiwa! Lengo lolote lile litakaloazimiwa kwa kutumia mbinu hii ni lazima litafanikiwa! Ufuatao ni ufafanuzi mfupi wa Mbinu hii:- S=Specific M=Measurable A=Attainable  R=Realistic  T=Time 1. Specific (lengo lako liwe Mahususi) Lengo lazima liwe na sifa ya umahususi! Ni lazima useme kwa uwazi ni kipi unachokitaka! Kwa mfano huwezi ukasema ninataka nitengeneze kiasi kingi cha fedha! Kingi ni nini labda? Je unaweza ukafafanua maana ya kingi ukaeleweka kwa watu? Rafiki hakikisha unaazimia lengo ambalo ni mahususi ili iwe rahisi kufuatilia maendeleo yake pamoja na kujua kuwa umepata kile ulichokuwa unakitaka! Kwa mfano unaweza ukasema ninataka nitengeneze kiasi cha fedha taslimu 300,000/= kila mwezi! 2. Measurable (Lengo lako liwe linapimika) Lazima uazimie lengo linalopimika ili iwe rahisi kulitekeleza! Kwa mfano ukisema nataka niwe tajiri unamaanisha nini? Je, unataka uwe tajiri wa nini? Je, unat...

Je, Unataka Kudumu Katika Kufanya Tabia Nzuri Muda Wote! Kama Jibu Lako Ni Ndiyo Soma Hii...

Image
Ukweli mchungu ni kwamba tabia mbaya ni rahisi kuzitengeneza lakini ni ngumu kuishi nazo, ikiwa tabia nzuri ni ngumu kuzitengeneza lakini ni rahisi kuishi nazo... Unatakiwa kujua kwamba kila tabia unayoifanya ni kisababishi cha matokeo fulani miaka kadhaa ijayo... Na, matokeo hayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya. Hata hivyo uzuri au ubaya wa matokeo hayo utategemeana na aina ya tabia utakayoifanya! Rafiki unatakiwa kuweka akilini mwako kwamba, ukiweza kufanya baadhi ya tabia ndani ya kipindi fulani cha muda zitakutengenezea utambulisho.  Na kwa vile somo hili linazungumzia jinsi ya kudumu na tabia nzuri muda wote, basi endapo utadumu katika kufanya tabia hizo utadumu katika utambulisho ulio  mzuri! Ndugu, unaalikwa kuhakikisha kwamba unadumu katika kufanya tabia nzuri tu, ili zikusaidie katika kukufanya ubaki katika utambulisho ulionao, pamoja na kuendelea kupata matokeo mazuri ambayo umekuwa ukiyapata muda wote! Rafiki, unatakiwa kujua kwamba mafanikio siyo lengo l...

Sababu Kuu Tano Za Kwanini Unatakiwa Usome ujumbe Huu Ikiwa Ni Mwanzo Kabisa Wa Mwaka...

Image
Habari yako rafiki yangu! Karibu kwenye mwendelezo wa makala nyingine inayochambua kuhusu mambo ya msingi, unayotakiwa uyafahamu pamoja na kuyaishi kwa mwaka 2024 ili ubadili maisha yako! Jana lilidokezwa jambo moja tu, kwa leo utaenda kudokezewa mambo mengine matano ya msingi unayopaswa uyafahamu na kuyaishi!  Mambo hayo ni kama ifuatavyo:- 1. Unaweza Kuwa Yeyote Yule... Umekuwa hivyo ulivyo siyo kwa sababu ulipaswa uwe hivyo. Bali umekuwa hivyo kwa sababu kuna mifumo iliyokutengeneza na kukufanya uwe hivyo ulivyo.  Hii ni sawa kusema endapo utaamua, unaweza kuwa yeyote yule unayetaka uwe na hakuna mtu wa kukuzuia. Rafiki, dunia ni mali yako, kuwa unachotaka! Hutakiwi kufungwa na utambulisho wa kutengenezewa tena, badala yake sasa unaweza ukajitengenezea utambulisho wako mwenyewe, na kuwa yule unayetaka uwe... Unatakiwa kujua kwamba, hakuna kitu kitakachokusimamisha kuwa yule uliyeamua uwe. Leo hii huenda ukawa unatambulika kwa sababu ya kozi uliyosomea au kwa sab...