Posts

Showing posts from April, 2023

Kwanini Huwa Unapata Kinyume Na Kile Unachokiomba...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba zaidi ya asilimia 90 ya sala zinazoombwa na watu wengi huishia kuwaletea matokeo yaliyo kinyume na matarajio yao?  Kwa mujibu wa tafiti binafsi nilizofanya nimebaini kwamba, hili limekuwa ni tatizo linalowakumba watu wengi sana!  Huenda hata wewe umekuwa ukikumbana na tatizo hili, usijisikie mpweke kwani wapo watu wengi sana wanaokumbwa na changamoto kama yako! Habari njema ni kwamba makala hii inaenda kutatua kabisa tatizo hili ambalo huenda limekutesa kwa muda mrefu, na umekuwa ukijiuliza maswali mengi pasipo kupata majibu muafaka! Kwa mfano huenda ukawa u memuomba Mungu akujaalie utele katika jambo fulani, halafu ukaishia kupata ukomo! Na kinachokuvunja Moyo zaidi ni pale unapotambua fika kabisa kwamba, Mungu wetu ni tajiri na vitu vyote ni mali yake! Sasa inakuwaje Wewe unakuwa siyo sehemu ya utajiri huo? Je ni kweli kwamba Mungu anakuwa amekutenga? Je ni kweli kwamba Mungu anakuwa hakujali? Je ni kweli kwamba...

JINSI YA KUJIONGEZEA NA KUJITENGENEZEA THAMANI SOKONI....

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba thamani ya mtu ndiyo hupima hadhi yake pamoja na kipato anachoweza kukitengeneza?  Unatakiwa kujua kwamba utabadili maisha yako siku utakayoamua kuongeza thamani Yako! Na kama hutoamua Kujiongezea  thamani hakuna atakayekufanyia hivyo!  Hata hivyo unatakiwa kujua kwamba, siku ambayo thamani yako itapanda, ndiyo siku ambayo ulimwengu utakutambua wewe ni nani! Hakuna kipya chini ya jua, maandiko matakatifu yanasema hivyo!  Hii inamaanisha kwamba kwa chochote kile utakachokifanya, tayari kuna watu walishafanya, lakini pia kuna wengine ambao wanafanya kitu hichohicho na kwa namna moja ambayo hata wewe unafanya!  Hivyo basi ili kufikia hatua ya kutambuliwa na watu wengine, ni lazima uwe umejiongezea thamani kubwa sana, kiasi kwamba utaweza kutofautishwa na wengine!  Kwa ujumla thamani ni kipimo rasmi ambacho, humstahilisha, humheshimisha pamoja kumtambulisha mtu! Je, kwa namna unavyojiona, wewe ni m...

How To Build Yourself And Increase Your Value In The Market...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e   Do you know that the value of a person is what measures his status with the income he can make?  You should know that you will change your life the day you decide to increase your value! And if you decide to add value to yourself, no one will do it for you!  However, you should know that, the day your value increases, is the day the world will recognize who you are! There is nothing new under the sun, the scriptures say so!  This means that whatever you are going to do, there are already people who have done it, but there are also others who are doing the same thing and in the same way that even you are doing it!  So in order to reach the point of being recognized by other people, you must have added a lot of value to yourself, so much so that you will be able to be distinguished from others!  In general, value is an official measure that qualifies, honors and identifies a person! In the way you see yourself, are ...

Je Ni Namna Gani Ninaweza Kutawala Vema Matumizi Ya Muda Wangu...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Sote tumekuwa na muda wa kutosha kabisa wa kutuwezesha tuishi maisha yenye mafanikio! Cha ajabu na kinachosikitisha zaidi wengi wetu tumeshindwa kuyafikia mafanikio hayo kutokana na kushindwa kuutumia vyema muda wetu!   Ukifanya upembuzi yakinifu utagundua kwamba wengi wetu tupo nyuma ya muda! Kwa mfano kwa siku ya leo sote tumepewa muda sawa, ambayo ni masaa 24, lakini kila mtu alivyotumia masaa hayo anajua yeye! Ukija kwangu mimi nimetumia baadhi ya muda kwenye hayo masaa 24, kukuandikia wewe ujumbe kuhusu namna ya kutumia muda wako kwa usahihi! Mpenzi msomaji unatakiwa kujua kwamba, unahitaji kujitawala mwenyewe ili uweze kutumia muda wako kwa ufasaha! Zifuatazo ni mbinu zitakazokusaidia ili uweze kutumia muda wako kwa ufasaha:  1. Anza na Mungu kwanza: (Labda uwe huamini katika Mungu, na ninakupa pole sana Kama huamini katika Mungu!) Njia nzuri ya kwako wewe kutumia muda wako ni kupitia kuanza na Mungu kwanza! Tenga muda wa ku...

Mambo Matano Unayopaswa Uyafahamu Kuhusu Muda...

Image
Na Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba muda ni rasilimali ambayo inaweza kuwekezwa? Huenda ukawa hulifahamu jambo hilo, ndiyo maana umekuwa ni muumini wa kutumia muda kiupotevu pasipo hata kujua kwamba kuna sehemu ya muda wako unaipoteza! Zifuatazo ni hoja zenye mashiko kuhusu muda! 1. Muda ni maisha! Muda ndicho kipimo halisi  cha hadhi ya maisha ya kila binadamu. Kwamba kutoka siku umezaliwa mpaka sasa, umeweza kuishi ndani ya kipindi cha muda fulani!  Hivyo basi hadhi ya maisha utakayokuwa nayo itathaminishwa kwa kuhusishwa na kipindi cha muda ulichoishi. Hata hivyo hadhi utakayokuwa nayo ndicho kitakuwa kipimo halisi kinachoonesha matumizi yako ya muda yapoje! Kwa mfano tufanye labda umeishi kutoka 1990 hadi 2030.  unachopaswa kujua ni kwamba, utakuwa na hadhi fulani kimaisha kadri ya muda uliotumia kuishi pamoja na namna ulivyotumia muda wako! Jaribu kufanya uchunguzi, utajua kwamba kuna baadhi ya watu wana umri mdogo lakini wamepiga hatua nd...

Muda Hutufundisha Thamani Ya Maisha...

Image
 Na Emmanuel Samuel King'ung'e Usipotumia muda wako katika kufanya mambo ya msingi, basi mambo yasiyo ya msingi ndiyo yatatawala matumizi ya muda wako! Uelewa  kuhusu muda bado upo katika kiwango cha chini sana miongoni mwa watu wengi, na hii ndiyo sababu kubwa watu wengi hutumia sehemu kubwa ya muda wao kufanya vitu visivyokuwa na thamani kabisa au vyenye thamani ndogo! Je muda wako wote wa thamani ulionao huwa unatumia kufanya nini? Kumbuka, ili jambo fulani liweze kutokea ni lazima lifungamane na kipindi fulani cha muda! Hii inamaanisha pasipo uwepo wa muda hakuna chochote kile kitakachotokea! Hivyo basi endapo utakuwa hauna chochote cha maana unachokifanya kwenye matumizi ya muda wako,  hakuna matokeo ya maana  utakakayoyapata maishani mwako! Unatakiwa kujua kwamba wengi wetu huwa tunaishia kuwa watu wa kawaida, pamoja na kupata matokeo ya wastani kutokana na namna tunavyotumia muda wetu! Weka suala hili akilini mwako, daima muda huwa ndiyo kizuizi ch...

Unahitaji Kuamua Vyema

Image
Hivi unafahamu kwamba hapo ulipo pamoja na hivyo ulivyo leo ni matokeo ya maamuzi yako uliyofanya jana? Unatakiwa kujua kwamba Kwa chochote kile kinachotokea maishani mwako kinaendeshwa na maamuzi. Hivyo basi endapo hakutakuwa na maamuzi yatakayofanywa hakuna chochote kile  kitakachotokea... Na ndiyo maana kanuni ya kichocheo na matokeo inasema kwamba " kila matokeo yana kichocheo chake" Hii inamaanisha kwamba maamuzi utakayoyafanya ndiyo yatakuwa kama kichocheo, halafu kile utakachokipata baada ya kufanya maamuzi ndicho kitakuwa matokeo yenyewe! Mbali na hilo huna budi kufahamu kwamba, vile  utakavyokuwa kesho itategemeana na maamuzi utakayoyafanya leo! Kutokana na ukweli huo ninawiwa kukufamisha kwamba, ni muhimu kufanya maamuzi ya busara leo hii, ili kesho yako ije ikushukuru kwa maamuzi uliyoyafanya jana! Vilevile unatakiwa kujua kwamba ukishindwa kufanya maamuzi sahihi utaishia kulaumu. Mbali na kulaumu sana unapaswa kujua kwamba hakuna utakachobadili, kwani ...

Jinsi Ya kufanya Maamuzi Sahihi Kwa Ajili Ya Kesho Yako

Image
Na mwandishi Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba kile unachoamua kufanya leo ndicho kinachopima vile utakavyokuwa kesho? Unatakiwa kujua kwamba hapo ulipo na hivyo ulivyo ni kutokana na maamuzi yako mwenyewe! Aidha uliamua mwenyewe au kuna mtu alikuamlia na wewe ukakosa chaguo mwisho wa siku ukajikuta, ukiamua pasipo kutumia dhamiri yako hali ambayo imekuletea matokeo mabaya! Kitu kimoja cha msingi unachopaswa ufahamu ni kwamba, ili uweze kupata matokeo ambayo hukuwahi kuyapata ni lazima ukubali kufanya maamuzi ambayo hukuwahi kufanya! Hata hivyo unatakiwa kujua kwamba siyo kila uamuzi ni uamuzi na siyo kila anayeamua anaamua kwa usahihi! Kwani kutokuamua ni kuamua pia, maamuzi yasiyo sahihi nayo ni maamuzi pia maamuzi sahihi ni maamuzi! Sababu kubwa ambayo imetufanya wengi tubaki kuwa watu wa kawaida, ilihali ndani yetu tunamiliki kitu kisicho cha kawaida ni aina ya maamuzi tunayoishia kuyachagua! Unatakiwa kujua kwamba, haujaumbwa uishie kuwa mtu wa k...

Kile Unachokijua Ndicho Kitapima Umbali Utakaoenda Kimaisha

Image
mwandishi Emmanuel Samuel King'ung'e Hivi unafahamu kwamba moja ya adui tishio sana wa binadamu katika kizazi hiki tulichonacho leo ni ujinga? Kama ulikuwa hujui basi leo leo ukweli unaenda kufahamika... Unatakiwa kujua kwamba hata baba wa taifa hayati  Mwl J. K. Nyerere aliutaja ujinga kama miongoni mwa wale maadui watatu wakubwa wa taifa letu pendwa la Tanzania... Hii inamaanisha ujinga lilikuwa janga la taifa toka enzi hizo... Lakini cha kushangaza zaidi ni kwamba kadri siku zinavyozidi kwenda mbele ndivyo tatizo hili linavyozidi kukua na kwenda hatua mbaya zaidi...  mategemeo yangu makubwa yalikuwa ni kuisha kwa tatizo hilo kadri siku zinavyozidi kwenda lakini hali imekuwa kinyume chake... The situation is getting worse as long as the days moves on... Moja ya kitu ambacho natamani hata leo kingeondoka kwenye jamii yangu ni ujinga.. Natamani ujinga ungeondolewa kwa nguvu zote kutokana na giza linalosababishwa na ujinga hasa kwenye Fahamu za watu wengi... Unataki...